BILA
MABADILIKO ITAKUGHARIMU
Unapoanza mwaka
usidhani unaanza kwa bahati mbaya tu. Sikiliza naomba unielewe vizuri, wapo
wangapi kama wewe hawakuweza kupita mwaka lakini wewe umepita si tu kwamba
umestahili. Ngoja nikueleze unajua kukaa duniani pia ni majaribu maana kuna
hesabu inatakiwa kutolewa mbele za Bwana wetu Yesu Kristo. Hivyo natamani
uelewe kuwa kuna majukumu ambayo Mungu ameyataka kwako yatendeke yasiofanania
na wengine.
Tunaposoma Mt
25:14-30 tunaona watumwa waliopewa talanta na Bwana wao alipokuwa akisafiri
wakafanyie kazi. Ili kila mmoja alete ujira wake sawasawa na namna
walivyotumika hata Bwana wao atakaporudi. Walipewa mmoja talanta tano, mwingine
mbili na mwingine moja na biblia inasema kila mmoja sawa na kadiri ya uwezo
wake.
Ina maana gani?
Bwana wao ni Yesu Kristo, watumwa ni mimi na wewe na talanta ni vipawa, karama
au makusudi ya Mungu. Utagundua talanta hizi walipewa kwa idadi isiyofanana hii
ina maana makusudi ya Mungu kwa watu hayafanani hivyo usije ukaiga kusudi la mwenzio
itakugharimu. Maana Bwana alitoa hiyo talanta anajua ya kuwa hakuna mwingine
aliyepewa talanta kama yako. Ukiiga ya mwingine utashindwa kuzalisha ya kwako.
Na ndio maana watu hawafanani kimajina ili kutofautisha makusudi ya Mungu
katika maisha yetu.
Kama biblia
inavyotueleza hivi leo umeingia mwaka mpya jiulize nafanya nini utagundua
haukuingia kwa bahati mbaya. Fikiria gari alilopanda mwenzako ndio hilo
unalopanda wewe lakini yeye alipata ajali mpaka kufa, chakula anachokula
mwingine ndio hicho unachokula wewe lakini mwenzio kapelekwa kwa operation.
Haya ni mambo ya ajabu yahasimuliki kwa kirahisi mno lakini ngoja nikueleze
hukuja duniani kushangaa magari na magorofa wala kushabikia wengine.
Wewe ni sawasawa na
mchezaji uwanjani. Una namba yako na hiyo namba yako haifanani na mwingine
usipocheza vizuri katika namba yako maana yake utapelekea timu kushindwa na
hata hivyo kocha kwa sababu anataka kuimarisha timu akigundua wewe ni mwenye
makosa utakaa benchi tu. Kwa huruma kocha huweza kukupa muda wa kubadilika
usipobadilika basi anakutoa maana sabu zipo nyingi.Hivi uliwahi kujiuliza kwa
nini hatuna Yesu wengi duniani waokoe watu hii ni kwa sababu kila alie kuja
duniani alikuja kwa mpango kamili.
Ngoja nikuambie kuna
watu wanafanya mambo ambayo Mungu hakuwaagiza na hiyo itawagharimu wengi sana
maana wanashulika sana na mavazi, kula, kunywa, kusoma, kazi, mume, mke au
watoto na vingine vyenye mfano na hivi. Kumbe wanajiangamiza wenyewe maana sio
talanta waliopewa.
Nataka ulewe kuwa
katika mwaka Mungu ambao amekupa kuna kuongezeka na kupungua pia hebu
tutatazame nini kilitokea Bwana wao aliporudi biblia inasema katika Mt 25:19-30
tunaona majibizano kati ya wale watumwa na Bwana wao aliporudi. Wale
waliozalishwa walibarikiwa na kuongezewa lakini yule mmoja ambaye hakuzalisha
alipokonywa na kupewa aliozalisha 5 ziada kisha akatupwa kwenye giza ambako
ndiko kuliko na kilio na kusaga meno.
Ndugu yangu jifunze
kunyenyekea acha kuishi kwa mkumbo itakugarimu. Utaratibu wa Mungu ni kwamba
una gharimika kwanza kisha anakubariki lakini utaratibu wa shetani unabarikiwa
kwanza kisha gharama baadae. Sikiliza kile Mungu anachokufundisha badilika anza
kuzalisha.
Barikiwa sana
Na Henry
Nicholaus
MITEGO YA
ADUI
Tukubali tukatae
tunae adui naye ana mawakala wake. Kama Mungu naye alivyo na mawakala wake
maana shetani amekopi na kupesti utaratibu wa Mungu na hata mfumo wa serikali
yake. Naye kila siku hutega mitego. Kama huwezi kutegua mitego huwezi kuishi
maisha ya ushindi. Katika mitego kuna umaskini, magonjwa, kufungwa ufahamu,
uvunjifu wa ndoa, kufeli, uzinzi n.k
Mitego hiyo huweza kufanyika kwa maneno yako au maneno ya wengine Mith
6:2. Mitego inaweza ikategwa kutokana na vinywa vyetu. Wako wengine wako kwenye
magonjwa, madeni, matatizo mengine hii ni kwa sababu shetani amewatega.
Licha Ayubu kuishi
maisha yasiyo na dhambi bado shetani alimtega Ayu 22:10. Hiyo mitego ikiteguka
unakuwa huru. Mitego haiondoki kwa sababu unaichukia bali huondoka kwa sababu
unajua kuitegua. Unaweza ukategwa katika fedha zako, ukazila pasipo kutoa zaka.
Hivyo basi hizo pesa zinakuwa mtego kwako. Katika Eze 21:21 Mfalme wa Babeli
alikaa katika njia panda akaweka terafi (ni kipimo cha kichawi ambacho hutumika
kukamata watu na kuangalia nyota zao au kuwafanya chochote. Kwa mfano kupitia
terafi huweza kuangalia figo na kutia ugonjwa ndani kisha ukaanza kusumbuliwa
na gonjwa hata madaktari wasiweze kukupatia tiba.
Laana ya mizimu
hutokana na matendo ya shetani waliofanya baba zetu kwa kumtumikia. Kut 20:4-5
Kuna laana zinatutafuana lakini imejengeka kuwa ni mazoea kwetu. Laana
utaiagundua kwa matokeo. Ukiwa unapenda sana kukuna sikio ni moja wapo ya
ishara ya kutafunwa na laana za mizimu.
Isa 25:7 Ukatae uso wa stara maana kuna maisha ulionayo ambayo huwezi
kushangilia au kufurahi. Uso wa stara ni uso wa nuksi usiobadilika au wenye
mikosi.Ukiwa hata fedha haziwezi kuja kwako. Mal 2:3 Mungu akikemea mbegu kwa
ajili yako unakufa, unafilisika, unakopa ovyo, ulivyoanzisha vinakufa kama
biashara. Ukipakwa mavi katika uso wako hupatikibali. Katika ulimwengu wa roho
kuna watu wamepakwa mavi.
Uso wa sitara ni uso
mbaya sana. Laana ya mizimu ndio inayo vutia uso wa stara. Kama baba yako
hakununua baiskeli wewe utapakizwa boda boda katika maisha yako. Uso wa stara
hauondoki kwa kuomba, lazima ufundishwe na mtu mwenye ufahamu.
Ukiwa na utaji
unakuwa kama mtu aliyefunikwa na kitu usoni asiyeweza kuona vitu vizuri.
Unakuwa mtu wa kuiga huna mawazo au mtazamo wa kwako.Sisi hatuna kopi duniani.
Ndio maana unaweza ukakuta mtu analalamika anasema nchi hii haina pesa. Kumbe
yeye hana pesa ila nchi ina pesa. Ukiona mtu wa namna hii ujue ya kuwa uso wake
una utaji.Utaji ukivunjika kwko utajua mpango wa Mungu kkatika maisha yako.2Kor
3 ishara ya kuwa na utaji ni uzito wa kufikiria.
Hivyo ndugu yangu
kataa roho ya utaji kwa jina la Yesu na roho ya stara pia. Ili uweze kufanya
mambo yako kwa ustadi na weledi katika kumwamini Mungu .
Ubarikiwe
Na Henry
Nicholaus
MAOMBI
Maombi ni mtandao wa
kiroho ambao moja kwa moja hutuunganisha na baba yetu aliye mbinguni.
Maombi kwa mkristo
ni silaha pekee ambayo huitumia katika kupambana na kuyashinda majaribu
mbalimbali unayokumbambana nayo.
Lakini wakristo
tulio wengi hatujui jinsi ya kuomba hii ni sababu hatumruhusu Roho Mtakatifu
aingie moyoni mwetu na atawale maisha yetu ya kiroho tunakua na nia mbili Yak
4:4-5
Na wengi wetu
tunategemea vitu tuvipate kirahisi hali tukijua yupo mpangamizi wa
ulimwengu.Lakini hatuvipa kwa sababu hatuombi Yak 4:2.Pia katika maombi yetu
yatupasa kusemezana na Bwana Mungu wetu kwa unyenyekevu hali tukijua kuwa uwezo
na mamlaka ni katika yeye peke yake
Katika maombi
yatubidi tumsihi sana Mungu wetu ili atusaidie tuweze kuvaa vinywa vyenye
mamlaka.Hii ni kwa sababu kwa uamuzi wa kuwa mwana maombi.Awali ya yote
yakupasa kuwa na imani iambatanayo na matendo ili kutokana na imani
iliyojitosheleza tuweze kufikia kiwango cha juu cha maombi ambapo ndipo
tunapopokea mamlaka Efe 4:13 "Hata na sisi sote tutakapoufikia umoja wa
amani na kufahamu sana mwana wa Mungu hata kwa mtu mkamilifu hata kufika kwenye
cheo cha ukamilifu wa kristo".
Hivyo basi kama vile
jinsi Yesu alivyowafundisha wanafunzi wake kuomba si zaidi sana na sisi pia
tumwombe Bwana wetu Yesu Kristo azidi kutuonyesha jinsi ya kuomba .Amen
Barikiwa
Na Anotite Sanga
IKIMBIE
ZINAA
Mw 6: 1 - 5 Mungu
hukasirishwa sana na zinaa.Watu hawa katika kipindi cha Nuhu walipendezwa na
zinaa mno.Hivyo Mungu akaazimu awaangamize kwa maji.Lakini utagundua hii ni
hukumu ya pili.Lakini hukumu ya kwanza ilikuwa ni kupunguzwa kwa siku za
kuishi.Swali ambalo tutajiuliza kwa nini siku zipunguzwe?Hii ni kwa sababu watu
wanakumbatia dhambi na dhambi hiyo ni zinaa.Biblia inatufundisha kabla ya
kizazi cha Nuhu dhambi ilikuwepo Mw 4:8 -10.Lakini biblia haikutufundisha kuwa
Mungu alipunguza miaka.Hivyo tunajua dhambi ya zinaa ndio kigezo ambacho
kilimfanya Mungu apunguze siku za kuishi.Bado tunaweza kujiuliza kwa nini siku
zipunguzwe neno lake linatueleza kuwa zinaa ndio dhambi inayofanyika juu ya
mtu.Hivyo huleta unajisi wa Mungu maana miili yetu ni hekalu lake 1Kor 3:16
Hivyo basi tumekuwa
wanyany'anyi maana kusema nyumba yangu itaitwa nyumba ya sala lakini nyinyi
mmeifanya kuwa pango la wanyany'anyi Mt 21:13.Lakini wale wasomaji wa biblia
wataelewa kuwa Sodoma na Gomora iliangamizwa kwa sababu ya zinaa Mw 18:20 - 21,
19:1 - 8, Yuda 1:7.Ikiwa Mungu aliwatenda hivi Sodoma na Gomora ni kitu gani
kilichowafanya wanadamu wa leo amini kuwa Mungu amebadili mawazo yake juu ya
watendao uasherati? Yer 30:23,Wimb 2:7,Mith 6:23 - 26
1Sam 2:22 - 34
Hofini na Fenehasi walipangiwa kufa siku moja kwa sababu walifanya zinaa nao
bado walikuwa wakifurahia.Na hii ndio sababu Mungu anatuambia kuwa hawezi
kuchukuliana na mwanadamu afanyae mambo ya jinsi hii.Lakini Mungu anatufundisha
kwa habari ya siku za mwisho kuwa mambo yaliotokea kipindi cha Nuhu na wakati
wa kipindi cha Sodoma na Gomora nao yatokea pia katika siku za usoni 2Tim 3:1 -
6, kwa sababu tu wanawake wengi wanapenda fedha na anasa wamejikuta wakiingia
kwenye uzinifu.
Swali la kujiuliza
hivi ni kwa nini watu wanaelezwa kuwa uzinifu au uasherati ni mbaya lakini
wanaendelea.Hii ni kwa sababu kuwa wote hawana akili kabisa Mith 6:32.Tunaweza
kujiuliza kuwa sababu ya ujinga inatoka wapi?Roho wa Mungu anatueleza inatoka
Lk 8:9 - 14.Ni dhahiri kabisa palipo na zinaa kuna uharibifu kama
Ukimwi,kutokuolewa/kuoa,kuvunjika kwa ndoa,kufungwa kwa mfuko wa uzazi au
kutozalisha mbegu za uzazi na mwisho kabisa mauti na ndio maana shetani
anawekeza sana mambo haya katika movie,internet na muziki.Nilikuwa namwambia
mtu mmoja kilichobaki tu ni picha za ngono kuhalalishwa kuwa matangazo
halali,ili kubandikwa ukutani na kuonyeshwa kwenye video.
Nataka kukueleza
kuwa jambo hili halikuja kwako kwa bahati mbaya, na ndicho niwaambiacho watu
kuwa neno haliji ili ulisikie tu bali huja kwa mpango maalum.Hivyo hata habari
za kukimbia zinaa zimekuja kwako kwa mpango maalum1Kor 10:11.Kitu cha muhimu
upate kujua kuwa zinaa inakimbiwa ukitaka kuishinda lakini ukishindana nayo
utaanguka tuu na hii ndio sababu ya Yusufu kuchopoka wakati mke wa Potifa
alipokuwa akimlamisha kufanya zinaa Mw 39:7 - 12.Hivyo usijifanye komandoo
mbele ya zinaa 1Kor 10:12
Na Henry
Nicholaus
ISHI
KULINGANA NA NYAKATI NA MAJIRA YALIYOAMRIWA NA MUNGU KWAKO
Mhubiri 3:1-8
"Kila jambo
kuna majira yake na wakati.Kwa kila kusudi chini ya mbingu".Mhu 3:1
Wakati kwa kusudi
bali majira kwa jambo.
Kuna tofauti gani
kati ya wakati na majira? Wakati ni kipindi alichokuwa nacho mtu kwa ujumla
LAKINI Majira ni muda halisi uliopo ndani ya wakati.Wakati hubeba kusudi ambalo
hutimilika kwa kuzaliwa kwa majira ya mambo tofautitofauti yanayoleta ukamilifu
ya wakati huo.
Mfano wa kawaida
Vijana walio na umri
kwanzia miaka 12-18 kwa mtazamo wa kawaida wanatazamiwa kuwa katika wakati wa
kupata elimu ya sekondari LAKINI katika wakati huo hubeba majira mbalimbali
kama majira ya mitihani ili kuweza kupimwa na kufikia kusudi ambalo ni kumaliza
elimu hiyo,likizo kwa mapumziko na mengineyo
Kwa nini tuishi
kulingana na majira na nyakati zilizoamriwa kwetu?
Inapaswa Ijulikane
kuwa Mungu alitujua kabla hatujakuwapo kwenye ulimwengu huu,hivyo nyakati na
majira yetu katika maisha yalishapangwa au kuwekwa fixed Yer 1:4a
Sababu
i)
Sisi ni wawakilishi wa maisha haya tuliopewa na Mungu kwa ajili ya
utukufu wake hapa duniani.Hivyo
imetupasa kuyatumia kama ilivyo wakati na majira alivyotuamuru sababu
tutatoa hesabu siku ya mwisho ya habari ya uwakili wetu 1Pet 1:17
ii)
Kulingana na nyakati na majira kunatuwezesha kupata mafanikio aliyokusudia
Mungu kwetu Isa 48:17
Mungu awabariki
Na Salome .J.
Senkoro
JE UNA HABARI KUHUSU
TUKIO LA KUTISHA LINALOKUJA HIVI KARIBUNI?
DALILI ya mvua ni
mawingu. Mtu mwenye busara aliyeanika nguo zake nje, anapoona mawingu yametanda
kila mahali, anajua kwamba mvua wakati wowote inaweza kunyesha, hivyo anafanya
haraka kwenda kuzianua nguo hizo. Vivyo hivyo, Yesu Kristo anatuonya kwa msingi
huohuo, kuzitambua ishara za zamani hizi yaani dalili za nyakati hizi za
mwisho, au za mwisho wa dunia, na kuyajua yale yanayokuja ili tujiandae vema
kuyakabili. Biblia inasema katika MATHAYO 16:2-3, ”Akajibu akawaambia kukiwa
jioni, mwasema, kutakuwa na kianga; kwa maana mbingu ni nyekundu. Na asubuhi,
mwasema, leo kutakuwa na dhoruba; kwa maana mbingu ni nyekundu, tena kumetanda.
Enyi wanafiki, mwajua kuutambua uso wa mbingu; lakini, je ishara za zamani hizi
hamwezi kuzitambua?“ Sasa je, ni nini dalili za mwisho wa dunia?
Kilicho na mwanzo
kina mwisho, na mwisho wa dunia uko karibu sana. Dalili mbalimbali za mwisho wa
dunia, zinatajwa katika Biblia, kwa mfano katika MATHAYO 24:3-14; 1TIMOTHEO
4:1-5; 2 TIMOTHEO 3:1-5; na UFUNUO WA YOHANA 22:6-7,10-12. Dalili zote
zimetimia, na zinazidi kuwa dhahiri mbele ya macho yetu. Moja kati ya dalili
zinazotajwa ni wachafu kuwa wachafu na maasi kuongezeka (UFUNUO 22:11; MATHAYO
24:12). Kabla ya maangamizo wakati wa Nuhu na pia wakati wa Sodoma na Gomora,
uchafu uliongezeka sana. Vivyo hivyo siku hizi, tukiona mambo haya ya uchafu
yanaongezeka, tujue hiyo ni dalili ya mwisho wa dunia. Je, uchafu huu
umeongezeka hivi leo? Jibu ni kwamba, ni kwa namna ya kutisha.
Pamoja na sheria
kali ya kujamiiana, ambayo inawafanya watu wanaonajisi watoto wadogo, wabakaji
na walawiti, kupewa adhabu ya kifungo; bado vitendo hivi vinaongezeka kwa kasi
kama vile watu hawajali! Karibu kila siku tunasikia habari hizi katika vyombo vya
habari. Wengine wanaripotiwa kulawiti watoto wadogo waliowazaa wenyewe! Wengine
wanalawiti wazee wa miaka zaidi ya sabini! Wengine wanawabaka mama zao! Mtu
mmoja anaripotiwa kuwalawiti watoto wadogo watano wa shule ya msingi, zamu kwa
zamu! Sehemu mbalimbali duniani, wanaume wanaoripotiwa kuwaacha wake zao kwa
sababu hawataki kulawitiwa, wameongezeka sana. Huko Marekani na Ulaya, ndoa za
wanaume kwa wanaume (mashoga) na wanawake kwa wanawake(wasagaji) zimekuwa ni
jambo la kawaida. Waziri Mkuu wa nchi moja kubwa Ulaya, anataka ushoga
uhalalishwe na Bunge la nchi yake. Maaskofu wa dhehebu moja kubwa la Ukristo,
hivi karibuni, walipiga kampeni ya kutaka ushoga uhalalishwe! Wachafu watazidi
kuwa wachafu!
Dalili nyingine ya
mwisho wa dunia, inatajwa katika Biblia, ingawa haiko wazi sana katika tafsiri
ya Kiswahili. Katika Biblia ya Kiingereza ya tafsiri ya King James Version(KJV)
katika MATHAYO 24:7, tunasoma, …. ”…and there shall be famines and pestilences…..“
"Pestilences,“ ni magonjwa mabaya ya kuambukiza yasiyokuwa na dawa au
tiba. Leo tunaishi nyakati za kuwepo kwa Ukimwi, ugonjwa mbaya wa kuambukiza
usio na tiba. Hii ni dalili ya mwisho wa dunia.
Vivyo hivyo, dalili
nyingine inatajwa katika MATHAYO 24:14, ”Tena habari njema ya ufalme
itahubiriwa katika ulimwengu wote, kuwa ushuhuda kwa mataifa yote; hapo ndipo
ule mwisho utakapokuja.“Kwa kutumia teknolojia ya kisasa, Injili inahubiriwa
kwa kasi ya kutisha. Kwa mfano kwa kutumia ”satellite“, Mwinjilisti mmoja
anayeitwa Billy Graham, tarehe 14 April 1996, alihubiri Injili na nchi zote
ulimwenguni walisikia Injili kwa wakati huohuo, wakati yeye akiwa Marekani.
Hatusemi kwamba mwisho wa dunia utakuwa leo au kesho. Siku ile wala saa, hakuna
aijuaye, lakini yote haya ni mawingu ambayo ni dalili ya mvua! Maana yake ni
kwamba, tuko ukingoni kabisa na wakati wowote ule mwisho wa dunia unakuja!
Mwisho wa dunia
utakuwaje? Mfululizo wa matukio ya mwisho wa dunia, utatanguliwa na tukio la
kutisha litakalotokea ulimwenguni wakati wowote kuanzia sasa, maana dalili za
mwisho huu tumekwisha kuona kwamba zinatimia machoni petu hivi sasa. Tukio hili
, linaitwa ”Kunyakuliwa kwa watu waliookoka“, na linaelezwa katika 1
WATHESALONIKE 4:15-17, "Kwa kuwa twawaambieni haya kwa neno la Bwana,
kwamba sisi tulio hai, tutakaosalia hata wakati wa kuja kwake Bwana, hakika
hatutawatangulia wao waliokwisha kulala mauti. Kwa sababu Bwana mwenyewe
atashuka kutoka mbinguni pamoja na mwaliko na sauti ya malaika mkuu, na
parapanda ya Mungu; nao waliokufa katika Kristo watafufuliwa kwanza. Kisha sisi
tulio hai, tutanyakuliwa pamoja nao katika mawingu, ili tumlaki Bwana hewani;
na hivyo tutakuwa pamoja na Bwana milele…“
Kunyakuliwa, ni tendo la kuchukuliwa kwa kitu
ghafla, kwa kasi kubwa na kuondolewa pale kilipokuwa; katika hali ya kuwaacha
watu wamepigwa butwaa, kwa jinsi wasivyoweza kukipata kitu hicho tena. Watu
waliookoka, muda si mrefu ujao, watanyakuliwa kwa jinsi hii na Yesu Kristo.
Yesu anakuja kufanya kazi hii, haraka wala hatakawia (WAEBRANIA 10:37). Siku ya
kunyakuliwa kwa watu waliookoka, sehemu nyingine dunia itakuwa usiku, sehemu
nyingine mchana, maana majira duniani yanatofautiana. Jua likitua sehemu moja
ya dunia, linachomoza sehemu nyingine ya dunia.
Wakati wa
kunyakuliwa kwa watu waliookoka, ikiwa ni mchana, watu wote waliokufa tangu
zamani za kale wakiwa wameokoka na wakawa wamekwenda mbinguni, watafufuliwa na
kutokea duniani tena. Kila mmoja atawaona. Watakuwepo watu wengi kwa ghafla,
mitaani kila mahali, waliokufa zamani wakiwa wameokoka. Hata kama kwenye
makaburi ya zamani, siku hizi kuna Jengo la ofisi, watatokea humo humo ofisini.
Dakika moja kufumba na kufumbua, watu waliookoka ambao wako hai duniani nao
wataungana pamoja nao, na wote watabadilishwa miili yao na kupewa miili ya
utukufu wa milele, isiyoharibika. Biblia inasema katika 1WAKORINTHO 15:52-53,
”Kwa dakika moja, kufumba na kufumbua, wakati wa parapanda ya mwisho; maana
parapanda italia, wafu watafufuliwa, wasiwe na uharibifu, nasi tutabadilika.
Maana sharti huu uharibikao uvae kutokuharibika, nao huu wa kufa uvae
kutokufa.“
Katika wale watakaokuwako duniani, watatwaliwa
wale waliookoka tu na kuishi katika utakatifu mpaka mwisho. Watakuwepo wawili
wakilima kondeni au shambani, mmoja ameokoka na mwingine hajaokoka, ni mwenye
dhambi. Aliyeokoka atatwaliwa, ambaye hajaokoka ataachwa. Ikiwa ni katika basi,
treni au eropleni; dereva au rubani ameokoka, atatwaliwa, na wenye dhambi
watabaki. Tunasoma katika MATHAYO 24:40-41, ”Wakati ule watu wawili watakuwako
kondeni; mmoja atwaliwa, mmoja aachwa; wanawake wawili watakuwa wakisaga, mmoja
atwaliwa, mmoja aachwa.“
Ikiwa itakuwa usiku, na katika familia fulani
mume hajaokoka, mke ameokoka, watoto wakubwa hawajaokoka, na wako watoto wadogo
wasiojua mema na mabaya; mume huyo mlevi anayempiga vita mkewe kwa sababu
ameokoka, ataamka asubuhi na kushangaa kuona mkewe kitandani na watoto wadogo
hawapo. Atawauliza watoto wakubwa, Mama yenu yuko wapi?“ watajibu, ”hatujui“.
Atatoka nje kwenda kuuliza, na kila mahali itaripotiwa Polisi, kwamba wako watu
waliotoweka usiku, pamoja na watoto wote wadogo. Katika kituo cha Polisi pia,
kutakuwepo na polisi waliotwaliwa. Baada ya uchunguzi duniani kote, waandishi
wa habari ambao hawajaokoka, walioachwa, watatoa ripoti katika magazeti,
”Mamilioni ya watu kote duniani wameripotiwa kutoweka usiku wa jana. Uchunguzi
umeonyesha kwamba waliotoweka ni walokole ambao wamekuwa wakidhaniwa kuwa
wamechanganyikiwa au ”kupotea.“ Taarifa zaidi zinaeleza kwamba watoto wadogo
wote pia wametoweka. Taarifa za uchunguzi zinaonyesha kwamba waliotoweka
wamenyakuliwa kwenda kumlaki Yesu mawinguni kama walokole walivyokuwa
wakihubiri!“
Hawa watakaotwaliwa, wataungana na wale
waliofufuliwa, na kisha wote kwa pamoja; watavutwa kama kwa sumaku, kwa mvuto
utakaotoka kwa Yesu atakayekuwa mawinguni. Yeye hataonekana kwa wale
watakaokuwako duniani. Wenye dhambi nao watajaribu kupaa, haitawezekana.
Itakuwa kama kuku na ndege wanaposhitushwa na kishindo. Ndege hupaa angani,
lakini kuku akijaribu kupaa huishia kwenye kichanja cha kuanikia vyombo! Sumaku
itawavuta waliookoka tu, kama jinsi sumaku inavyovuta vyuma tu na kuacha
mchanga au udongo! Baada ya wenye dhambi kuachwa, ndipo kitakapokuwapo kilio na
kusaga meno hapa duniani. Itafuata dhiki kubwa ya miaka saba, ambayo namna yake
haijawahi kutokea. Biblia inasema katika MATHAYO 24:21, ”Kwa kuwa wakati huo
kutakuwapo dhiki kubwa, ambayo haijatokea namna yake tangu mwanzo wa ulimwengu
hata sasa, wala haitakuwapo kamwe.“ Wenye dhambi watateswa kwa namna ya
kutisha. Watu watatamani kufa kutokana na mateso na maumivu, lakini mauti
itakuwa imeondolewa (UFUNUO 9:2-6). Wataiambia milima na miamba, tuangukieni,
watamwomba Mungu awahurumie, huruma na uvumilivu wake utakuwa umekoma (UFUNUO
6:15-17; ISAYA 26:16-18). Wale walionyakuliwa huko juu watakuwa katika karamu
ya Arusi ya Mwanakondoo baada ya kupewa kila mtu taji zake (UFUNUO 19:5-9;
2WAKORINTHO 5:8-10).
Mpendwa msomaji,
parapanda inaweza kulia usiku wa leo. Je, utakuwa kundi lipi? Utanyakuliwa au
utaachwa? Ikiwa wewe ni mwenye dhambi, hujaokoka, utaachwa kwa hakika. Hata
hivyo, bado una nafasi ya kutubu dhambi zako. Ukifanya hivyo huku ukimaanisha
moyoni kuziacha dhambi zote, utasamehewa sasa hivi, na hivyo kuokoka. Na sasa
hivi utahesabiwa kuwa miongoni mwa wale watakaonyakuliwa (MITHALI 28:13; LUKA
1:77). Je uko tayari kutubu, na kuokoka? Najua uko tayari. Basi fuatisha sala
hii fupi kwa dhati kutoka moyoni:
”Mungu wangu, asante
kwa kunipa ujumbe huu kabla tukio hili halijatokea. Natubu dhambi zangu zote
nikimaanisha kuziacha. Yesu Kristo naomba unisamehe dhambi zangu zote na
kuniokoa. Naamini sasa kwamba umeniokoa, katika Jina la Yesu. Amen.“
Tayari umeokoka. Ili
uutunze wokovu wako mpaka wakati wa Kunyakuliwa, hakikisha unahudhuria
mafundisho katika Kanisa linalohubiri wokovu (ZABURI 119:11).
MUNGU AKUBARIKI!!!
Na Henry Nicholaus
SPEAK THE
WORD OF GOD IN A LOUD VOICE SO THAT IT CAN CAUSE EFFECT IN YOUR LIFE
"Kitabu hiki
cha Torati kisiondoke kinywa mwako bali yatafakari maneno yake usiku na mchana
upate kuangalia kutenda sawasawa na maneno yote yalioandikwa humo maana ndipo
utakapoifanikisha njia yako kisha ndipo utakapositawi sana" Yos 1:8
Tunapoutafakari kwa
kina sana mstari huu tuna mengi ya kujiuliza.Kuna mahusiano gani ya neno la
Mungu kuwa kinywani mwako na kufanikiwa au kustawi kwa mtu.Uwepo wa neno la
Mungu kinywani husababisha kinywa kuwa na mamlaka ya uumbaji.Mamalaka hayo ya
uumbaji ndio ambayo huzaa ustawi na mafanikio.Tunaposoma Mw 1:3 Mungu akasema
na iwe nuru ikawa nuru.Tunaona nuru ilikuja kwa sababu ya lile neno liliotamkwa
kutoka katika kinywa cha Mungu.Na ukizidi kufuatilia utagundua kuwa huu ndio
utaratibu ambao Mungu aliutumia katika uumbaji isipokuwa wa mwanadamu.
Kinywa kina nguvu ya
uumbaji unapotaka kufanikiwa tamka hilo neno ulilolisikia kwa sauti kupitia
kinywa chako mwenyewe.Huweza kubadili hali uliokuwa nayo hata kama kwa hali ya
kawaida unaona ya kuwa ni ngumu kubadilika.Mahali pengi maandiko yanatueleza kuwa
neno la Mungu lina nguvu katika vinywa vyetu Zab 33:9 inatoa ufafanuzi juu ya
jambo hili.
Yamkini u
mgonjwa,kipofu,huelewi darasani,hamna amani katika familia yako au una matatizo
mengi yaliokukumba.Hebu fanya uamuzi usio na majuto wa kutafuta neno la
kukuvusha kisha liseme kwa kinywa chako kwa kurudia rudia mara kadhaa.Au
kumbuka neno lolote ambalo uliwahi kulisikia hapo awali ambalo lahusu mazingira
kama hayo.Kisha litamke kwa sauti ili upokee matokeo.
Na ndio maana
shetani hulinyakua neno la Mungu ndani ya mtu asipolielewa.Hii ni kwa sababu
anajua kuwa pindi atakapoliacha neno kwa mtu litazaa.Hivyo huliondoa mara moja
ili lisizae matunda Mt 13:12-19.Maana tabia ya neno ni kuzaa pale
linapoachiliwa.
Tazama Mt 13:35
inasema ili litimie neno lililonenwa na nabii akisema.Jiulize huyu nabii
alinena hilo neno lini lakini mara baada ya miaka mingi neno litatimia na ndio
maana nilikueleza kuwa tabia ya neno ni kutimilika linaposemwa bila kujali ni
kwa kipindi gani litatokea.Lakini sharti litokee hata hivyo pasipo kujua sisi
kama vijana tumekuwa tukijinenea maneno ya kushindwa,udhaifu,hofu na mengine
mabaya yakiwemo.Kujipa a.k.a tusizozifahamu maana yake bila kujua maana ya
maneno yale yana athari kubwa katika maisha yetu.
Wewe leo unawaza
kujinenea nini?Kumbuka ardhi na mbingu huweka rikodi ya maneno yetu hivyo
wakati uliokusudiwa unapofika ni lazima hilo neno litimie.Unaweza ukasikia
mzazi anamwambia mwanae wewe ni kichaa na maneno mengine mengi lakini
inawezekana wewe ni mmoja wapo ulieambia maneno hayo ama kama hayo lakini iko
damu isafishayo Ebr 9:14.Maana unaposoma Isa53:5 mstari wa mwisho unasema na
kwa kupigwa kwake sisi tumepona juu kuwa siku hii ya leo umepona lakini pale
unapofanya maamuzi ya kuamini na kumkabithi maisha yako Yesu anafuta maneno
yote mabaya maana kwake yeye ya kale yamepita tena yamefanywa kuwa mapya
Ubarikiwe
Na Henry Nicholaus
UTAWALA WA
DHAMBI NDANI YA MTU HULETA UTUMWA
Kila binadamu
atendaye dhambi mbele za Mungu ni chukizo mbele zake.Maana dhambi ni kinyume
cha adili (jambo sahihi) naye Mungu hupendezwa na yaliyo mema.Lakini bado
tunafanya maovu mbele za Mungu Yer 8:10 "Basi kwa hiyo nitawapa watu wengi
wake zao na mashamba yao,nitawapa wale watakaowamiliki maana kila mmoja hutenda
mambo ya udanganyifu".Tunanyany'anwa mamlaka tuliopewa na Mungu mwenyewe
kwa sababu tunamchukiza Mungu inatupasa tujue kuwa hasira ya Mungu juu ya sisi
tutendao maovu ni kubwa haistamiliki Yer 10:10
Wakristo wengi
tunajua kuwa tunaenenda njia ya uovu wakati huo huo tunajua kusudi la Mungu juu
ya binadamu ni kukaa katika mpango wa Mungu.Tunashindwa kuenenda katika hayo
kwa sababu hatuna akili ndani yetu tumelikataa neno la Bwana kila mara
tunapolipokea Rum 1:28,Mith 1:29,1Kor 5:34 tumwombe sana Roho atusaidie kutumia
akili tunayoipata ipasavyo maana ni wengi wanaotamani kulisikia neno na kupata
akili ya namna hiyo.Lakini sisi tunaoipata tunaidharau.
Tunaweza kukaa
katika mpango wa Mungu maana yeye ni Mungu wa rehema na wala si mchoyo wa
fadhili pia si mwepesi wa hasira Yona 4:2 .Utakapogeuka kuwa mwaminifu na
kuendelea mbele na wala si nyuma yeye ni wa haki hata akuondolee udhalimu
wote.Lakini tusiwe wa maneno tu.Maana tumekuwa tukitubu sana lakini hatupo
tayari kuachana na mwenendo wetu wa dhambi na hapa ndipo hasira ya Bwana
huonekana juu yetu Yer 8:6 Tunayaweza yote katika yeye atutiaye nguvu.
Amani ya Mungu iwe
nawe
Na Maria Lodrick
UMUHIMU WA
KUOMBEA NDOA ZA WAZALIWA WA KWANZA
Mimi sijui
unachoweza kufikiri juu ya somo hili lakini Mungu anataka kukufikirisha kwa
namna nyingine nami sielewi kuwa uliwahi kuwaza kwamba utafundishwa kitu kama
hiki, basi fuatana nami kwa karibu sana ili usikie kile Mungu anachotaka
kukufikirisha.Natamani ujifunze kujiombea mwenyewe ili Mungu akupe kuona
umuhimu na akupe nguvu za kuomba juu ya kuoa au kuolewa kwa mzaliwa wa kwanza
au juu ya ndoa yake.
Mtu mmoja aliyekuwa
na umri karibu miaka 60 alikuwa akishukuru Mungu kwa ajili ya sendoff na harusi
iliyotangazwa katika ukoo wao.Maana toka utotoni hadi utu uzima hakuwahi kuona
au kusikia sendoff na harusi halali katika ukoo wao.Hii ilitokana baada ya kuamua
kushughulikia tatizo lao kwa mtazamo wa mzaliwa wa kwanza.Ndipo Mungu akawajibu
mpaka mwaka 2010
Je unajua ya kuwa
hali ya ndoa na pia hali yakuoa na kuolewa kwa sehemu kubwa inapatikana kwenye
lango ambalo ni mzaliwa wa kwanza katika ukoo au familia husika.Na ndio maana
kuoa au kuolewa kwa mzaliwa wa kwanza kunakuwa shida na kupigwa vita kwelikweli
kwa kuwa wao ni lango na mkondo wa Mungu.
Je unajua baraka
moja wapo ya mtu kuwa mzaliwa wa kwanza kwa haki ni kupata msaada wa uongozi wa
Mungu katika kuoa na kuolewa kwake na hii ndio sababu Isaka alivyokuwa
anaachilia baraka za mzaliwa wa kwanza kwa Yakobo Mw 28:6 tunasoma ya kuwa
katika kumbariki alimwagiza akasema usitwae mke kwa binti za kanani
Unadhani kwa nini
iwe hivyo.Hii ni sababu si kila mwanaume/mwanamke ameandaliwa kwa ajili ya
mwenzi wa mzaliwa wa kwanza.Bali mwenzi wa mzaliwa wa kwanza ameandaliwa
kupitisha mtoto atakayebeba lango la haki la mzaliwa wa kwanza.
Naamini unakumbuka
jinsi kuoa kwa Yakobo kulivyokuwa kwa matatizo na katika mazingira ya kukatisha
tamaa.Shetani alikuwa anatafuta Yakobo asimwoe Raheli ili kukwamisha kuzaliwa
kwa Yusufu Mw 29:19 - 21,25 - 28,31,30:22 - 24
Sasa unaweza kuelewa
kwa nini hali ya kukosa mtoto katika ndoa ya Ibrahimu kulileta maamuzi mabaya
ya kuzaa na msichana wa kazi.Hii ni sababu shetani alitaka Ishmaili achukue
nafasi ya uzaliwa wa kwanza wa haki ambayo ni ya Isaka.Ni kweli Mungu alimwambia
Ibrahimu kuwa atakayetoka katika viuno vyake ndiye atakayekurithi Mw
15:4.Lakini si kwa kuzaa na mwanamke yeyote aliyemtaka yeye au kushauriwa na
mke wake.
Ishimaili alitoka
katika viuno vya Ibrahimu ni kwa nini basi Mungu alimkataa.Tofauti ya Isaka na
Ishimaili ni nini wakati wote wametoka katika viuno vya Ibrahim?Tofauti zao
zilikuwa ni tofauti ya matumbo ya mama zao waliowazaa.Ubora wa tumbo la Sara
ulikuwa kutoka kwa Mungu.
Sii kila tumbo la
kila mwanamke limeandaliwa kwa jinsi hii.Na kwa sababu hii ni rahisi mwanamke
anayeolewa na kijana aliye mzaliwa wa kwanza atakuwa na uwezo wa kumzaa Isaka
kwa ajili ya Mungu na kwa ajili yako.Tena ni muhimu kujua kuwa si kila msichana
atapata nafasi ya kuolewa kirahisi na Ibrahimu.Uwe na hakika kuwa shetani
atajaribu kuwasumbua wakina Hajira kwa Ibrahim ili kuvunja ndoa yake Mw 12:15 -
20.Na tena ikiwa msichana amempata Ibrahimu wake na kuolewa kwa msaada wa Mungu
usishangae ukiona tumbo lake likipata vita na kushindwa kuzaa.
Naamini sasa unaweza
ukaelewa kwa nini Sara alipata shida ya kuzaa kwa Ibrahimu wake na kwa nini
Rebeka alipata shida ya kuzaa kwa Isaka wake na kwa nini Raheli alipata shida
ya kuzaa kwa Yakobo wake na kwa nini Hana alipata shida ya kuzaa kwa Elkana wake?
Ni ili wasiweze
kupitisha wazaliwa wa kwanza wa haki ili Mungu apate kama lango katika kizazi
kilichokuwa kinafuata baada yao.Fuatilia mwenyewe kwenye biblia uone
hili.Utaona ya kuwa Sara alimzaa Isaka ,Rebeka alimzaa Yakobo, Raheli alimzaa
Yusufu na Hana alimzaa Samueli.
Pia utaelewa kuwa
Ibrahimu alipata mzigo mkubwa moyoni wa kuona ya kuwa mtoto wake Isaka anapata
msaada wa Mungu katika kuoa kwake.Ibrahimu alimuelekeza mfanyakazi wake
aliyemtuma kumtafutia Isaka mke kuwa Bwana Mungu wa mbingu aliyenitoa katika
nyumba ya babaangu yeye atampelekea malaika mbele yako Mw 24:7
Unadhani Ibrahimu
alijuaje hili ya kuwa Mungu wake amemtuma malaika kwa kazi maalum ya
kuhakikisha kuwa Isaka aliyekuwa mzaliwa wake wa kwanza kwa haki anapata mke
sahihi.Ni lazima Ibrahimu alikuwa anaomba juu ya kuoa kwa Isaka kwa mzigo sana
huku ajua umuhimu wa Isaka kama lango na hivyo Mungu hawezi kuruhusu aoe
mwanamke yeyote tu.
Shetani anawapiga
sana vita wazaliwa wa kwanza juu ya hili kiasi kwamba anawafanya wazae watoto
wao wa kwanza nje ya ndoa.Una mzigo gani moyoni mwako wa kuombea mzaliwa wa
kwanza wa kiume juu ya kuoa kwake au wa kike juu ya kuolewa kwake na juu ya
ndoa zao.
Ombea mzaliwa wa
kwanza
Na Henry Nicholaus
SISI NI
WAJUMBE WA KRISTO TUNAOTAKIWA KUISAMBAZA INJILI
Kama mkristo kamili
anayemtumikia Mungu ni wajibu wetu kuendelea kumtangaza Kristo ili pale
atakaporejea atukute tukifanya hivyo ili kukusanya kondoo zake.
Mt 24:44 - 51 Kabla
ya Yesu Kristo kupaa mbinguni alituahidi kuwa atatuletea msaidizi kwetu naye ni
Roho Mtakatifu ili aweze kutuongoza katika kumtangaza Kristo.
Kama katika mfano
ulioelezwa katika Mt 24:44 - 51, Mtumwa aliachiwa kazi ya kuwapa watu chakula
naye akakawia akidhani kuwa Bwana wake atachelewa kurudi.Vivyo hivyo sisi nasi
wakristo ni watumwa na watoto wa Mungu tulioachiwa agizo la kuwapatia watu chakula
cha roho ambalo ni neno la Mungu.
Hii ni kwa sababi
kadri siku zinavyozidi kusonga na kuyoyoma ndivyo jinsi gani Yesu anavyokaribia
kurudi kulichukua kanisa lake hivyo basi hatujui siku wala saa.
Kwa maana siku
atakaporudi Yesu atampa kila mtu ujira wake sawasawa na kazi yake na tukimaliza
kazi (sisi tulio watu wake) tutavalishwa taji ya uzima ambayo ni kutokana na
juhudi katika kulitangaza neno la Mungu, tukiongeza idadi ya wamfuatao ili kwa
pamoja tupate kuuona ufalme wa mbinguni ambao huanzia ndani ya mioyo yetu na mwishowe kwenda kuurithi ule uzima wa
milele
OMBEA
MZALIWA WA KWANZA ILI FAMILIA YAKO IPATE KUFANIKIWA
Kut 2:23 - 24 Wana
wa Israeli walikuwa katika kiwango fulani cha maisha, nao walimlilia sana
Mungu, naye Mungu akawajibu kwa staili ambayo hawakutegemea.Na sisi tunajiuliza
kwa nini ilimchukua Mungu utaratibu mwingine kabisa ambao hatukuufikiria.Lakini
tunapojua kile anachotufundisha tunajua kuna utaratibu ambao Mungu amejiwekea
yeye mwenyewe kwenye ulimwengu wa roho.Na moja
moja wa utaratibu huo ni wa mzaliwa wa kwanza.
Kut 12:13 Katika Kut
12 yote anazungumzia juu ya kila familia ichinje mwana kondoo na damu ya ke
ipakwe kwenye miimo ya milango na vizingiti vya juu.Akasema hiyo damu itakuwa
ni ishara kwao kwa sababu kuwa Mungu alipokuwa anawapiga pigo kwa wazaliwa wa kwanza
alipoiona damu pigo halikuwapata.Na pia shetani atakapoamua kulipiza kisasi kwa
ajili ya wazaliwa wa kwanza wa Israeli atakapoiona ile damu atashindwa kuingia.
Ile damu ilikuwa
ishara kwa wana wa Israeli.Hivyo Mungu alitaka wajifunze ile ishara wapate
kuelewa kilichopo ndani ya ile ishara.Maana katika ishara kuna ujumbe,
kuelekeza.Maana ishara haiji yenyewe bali ilikuja ili wana wa Israeli waiangalie na kuifuta inapokuwaelekeza.Kama
kibao kinaelekeza Moshi usiangalie Morogoro.Kibao kilicho juu ya mlango kilicho
na damu kinawaelekeza wapi?Kwa mzaliwa wa kwanza.
Ili waweze kujua
kuwa Mungu hashughulikii milango kama milango bali huwashughulikia wazaliwa wa
kwanza kama lango au kipitishio.Na ndio maana mzaliwa wa kwnza ni lango.Mungu
anapomtazama mzaliwa wa kwanza hamtazami kama tunavyo mtazama sisi, anamtazama
kama lango linaloitwa mzaliwa wa kwanza na linapewa majina ambalo linaweza
kupitisha vitu ama la
Nawe kama mwiisraeli
kama biblia inavyotueleza una mpango gani juu ya jambo hili.Muhimu kulizingatia
maana linachukua nafasi kubwa katika maisha yako na si tu maisha yako hata ya
familia yako.Hivyo fanya maamuzi sasa sawasawa na neno lilivyotufundisha.
Barikiwa sana
Na Henry Nicholaus
NGUVU KAMA
MATOKEO YA KUHIFADHI NENO LA MUNGU
Unapokuwa na neno
nguvu ni zao lake.Nguvu ni udhihirisho wa neno la Mungu ndani yetu.Au ni
matokeo ya kuhifadhi neno la Mungu ndani yetu.Imani chanzo chake ni
kusikia,unaposikia unapata udhihirisho wa neno ambao ni nguvu na hiyo hupelekea
kujenga imani.
Mdo 1:6-8
Udhihirisho wa nguvu huja kwa Roho Mtakatifu tofauti na vitu vingine neno
huhifadhiwa katika moyo na si akili.Fil 4:13 Paulo anasema mengi anayoyafanya
yasingekuwa katika uweza wake kama nguvu haipo ndani yake.Neno huanza kisha
nguvu hufuata.
Mith 24:5 Ili uwe na
nguvu ni lazima uwe na hekima yaani neno la Mungu.Kusoma neno la Mungu sio tija
lakini uwepo wa neno ndani ya moyo wako ndio tija.2Pet 3:5 Mbingu na nchi
zilifanya kwa neno la Mungu.Lile neno lilileta nguvu ya uumbaji.1Kor 1:24 Kristo
ni neno hivyo neno huanza na kisha nguvu hufuata
Gal 3:22 Imetupasa
kulijua neno la Mungu ili tuweze kupata nguvu.Neno lilmefunga kila kitu ndani
yake.Watu wengi wanataka fedha lakini hawataki chanzo cha fedha ambacho ni neno
la Mungu.Kol 1:29 Ukiwa na nguvu ndogo hata udhihirisho wa Mungu kwako huwa mdogo.Mungu
anataka tulisimamie neno lake.Neno ni chanzo cha ushindi 1Kor 15:55-57.Hivyo
ilitushinde majaribu ni lazima tuwe na neno la Mungu.Na hilo neno ni lazima
likubalike ndani yetu.
Gal 5:24 Neno
haliwezi kukaa ndani yako kama hujalikubali na ndio maana wamataifa hawana
ufalme wa mbingunin kwa sababu hawakulikubali neno la Mungu.Nguvu za Mungu
zinapotenda kazi ndani yako kunakuwa na udhihirisho wa nguvu ya Mungu.Ebr 4:12
Neno lina uweza wa kutuwezesha kushinda dhambi.Tunatenda dhambi kwa sababu
hatuna neno la Mungu.Ili uweze kuuteka ufalme wa mbinguni ni lazima uwe na
nguvu Mt 11:12
Tuaache kutafuta
makanisa,watumishi na ibada bali tulitafute neno la Mungu ili tupate nguvu za
kutawala vitu vyote.Maana kila kitu kimefungwa katika neno la Mungu.Hivyo Yesu
alisema utafuteni ufalme wa mbinguni na haki yake na vyote mtazidishiwa.
Ili uwe hai siku
zote ni lazima ushinde majaribu na hii hutokea pale tu neno la Mungu linapokuwa
limetawala ndani ya mioyo yetu.Hii ndio sababu kubwa iliyomfanya Yesu amshinde
shetani kila wakati na kila hali jisomee mwenyewe Mathayo sura ya nne yote utayaona
haya
Ubarikiwe
Na Joseph Luoga
NI KWA NINI
WATU HAWASIKII NENO LA MUNGU
Yn 8:47
"Yeye aliye wa
Mungu huyasikia maneno ya Mungu, hivyo ninyi hamsikii kwa sababu ninyi si wa
Mungu".
Binadamu wengi wa
leo wamekuwa wakisikia neno likihubiriwa kila pande za dunia, je mbona hatuoni
watu wakibadilika. Wakristo wengi wa leo maisha yao yapo mikononi mwa
shetani.Kwa kuwa shetani ndio usukani wao katika maisha yao, ni vigumu wao
kuabadilika na kuingiza neno la Mungu kwenye nafsi zao kwa sababu ya utumwa
ndani ya shetani.
Watu wa leo hawana
hofu ya Mungu ndani yao ila wanahisi kuwa wana hofu ya Mungu.Au hofu ya Mungu
katika midomo yao na sio nafsi yao. Hii ni kwa sababu shetani ametawala maisha
yao kiasi kwamba wamesahau ukuu wa Mungu. Kwani akili zao zipo gizani na shetani
anazidi kuziweka mbali na nuru ya Mungu kwa kuwapeleka gizani zaidi. Katika
maisha, asili ya binadamu siku zote ni kuwa na kinachomwongoza,hakuna binadamu
ambaye anaishi tu.
Na siku zote binadamu akiongozwa na Mungu
atafwata ya Mungu na akiongozwa na shetani atafuata ya shetani. Kwa kuwa
binadamu wamekuwa wakimfuata ibilisi wamejikuta wakivutiwa na tamaa za ibilisi
na kwa kuwa wamefumbwa macho hawaoni tatizo hivyo hata wakihubiriwa watasikia
lakini havita ingia katika nafsi zao. Kwani akili ikisikiliza yale mahubiri
wakati ikiwa chini ya shetani mtu huya puuzia na kuyaacha. Ukisoma Yn 8:42-47
Utaona jinsi Yesu alivyokuwa akijaribu kuwaelewesha watu jinsi akili zao
zilivyokuwa zimefumbwa ndio maana walikuwa huwasikii walichokuwa wakihubiriwa.
Je mwanadamu afanye
nini ili aweze kusikia neno kama Mungu anavyotaka. Siku zote ukiwa ndani ya
mfumo fulani au ukiwa mwanachama ni vigumu sana kuona au kujua makosa yako
mpaka utakapokaa nje nakuangalia ule mfumo utajua makosa yake. Basi ili uweze
kusikia maneno ya Mungu itakubidi ufute mfumo wote wa shetani ndani ya akili
yako hapo ndipo utakapokuwa unatawala akili yako na ndipo utakapobidi kumwalika
Mungu akamate upeo wako na aandae maisha yako na hapo ndipo utakapoona jinsi
gani shetani alipokuwa ametawala akili yako na alivyokufanya ufanye vitu vya
ajabu lakini kwa kuwa uliikuwa ndani ya mfumo wake ilikuwa ni vigumu kwa wewe
kuona na kujua.
Mungu akusaidie,
akutie moyo wa kutamani kufanya mapinduzi katika maisha yako na kuongozwa na
mfumo wa Mungu
Ubarikiwe
Na Frederick Apina
HAIJALISHI
NI NAMNA GANI ULIVYOFANYA MTIHANI WAKO BALI MAOMBI YAKO YANA NAFASI KUBWA
KATIKA KATIKA KUAMUA MATOKEO YAKO
"Nami nitakupa
wewe funguo za ufalme wa mbinguni na lolote utakalofunga duniani litakuwa
limefungwa mbinguni na lolote utakalolifungua duniani litakuwa mbinguni na
lolote utakalolifungua duniani litakuwa limefunguliwa mbinguni" Mt 16:19
Yesu anapoeleza
habari za ufunguo anatumia siri ya mamlaka ya maamuzi ndani yetu. Si watu wengi
wanajua kuwa Mungu huachilia watu wake kufanya maamuzi pamoja naye katika
dawati lake. Ni kweli yamkini ulivyofanya mtihani wako, kwa mtazamo wako huwezi
kufikia malengo yako. Lakini Mungu anapokutazamisha kwa habari za mamlaka ya
maamuzi uwe na uhakika kwa mamlaka haya kila kitu chaweza kubadilika.
Yer 32:27 inatuambia
hakuna jambo lisilowezekana.Na ndio maana aliweza kubadili Bahari ya Shamu kuwa
nchi kavu.Haikuwa rahisi kwa wana wa israeli kumuelewa Mungu.Kumbuka Mungu
aliwatoa utumwani akiwaambia atawapatia nchi yenye maziwa na asali lakini Mungu
alipokuwa akiwapeleka katika nchi ya ahadi, Farao aliwafuatilia kwa nyuma
akiwataka kuwarudisha hali wakijua hataweza kuwashika wakajikuta njia
wanayoishika imefungwa kwa mbele na bahari huku pembeni ikifungwa na
miamba.Basi katika hali ya kukata tamaa Mungu anageuza majonzi yao kuwa furaha
mara baada ya kutenga maji na kuwaamuru wapite.
Hata wewe yamkini
ikawa ngumu kwako kumuelewa Mungu.Kwa sababu kama kuomba, uliomba na kama kutoa
sadaka ulitoa.Ngoja nikuambie Mungu anataka kujitukuza katika maisha yako
yamkini hukuwa kumwona Mungu kwa macho katika maisha yako sasa amekuja
kujidhihirisha kwako usihofu bali fuata kile nichokueleza wakati huu.
Ninachotaka ni wewe
kuamini jambo hili.Je unadhani kama
Mungu tunayemuabudu aliumba dunia na vyote viujazavyo hivi hivyo vya kwako
kweli vitamshida?Imani ni kuwa na uhakika ya mambo yatarajiwayo ni bayana ya
mambo yasiyoonekana Ebr 11:1.Jijengee uhakika wa jambo hili ili kile
ulichokitazamia kiwe chako.
Ngoja nikueleze
maombi utakayoyasimamia yatabadili huzuni yako kwani yana nafasi ya kubadili
maksi,kusahihisha makosa na kutoa upendeleo kwa karatasi lako.
Ndugu yangu
unayesoma waraka huu natamani uamini neno hili kwani ni amini na kweli. Hata
mimi nilipokuwa nafanya mtihani wangu wa taifa niliingiza neno hili katika
uhalisia hatimaye Mungu alijiinua kwa viwango vya juu mno.
Nakutakia kila heri
Na Henry Nicholaus
MWENYE
KUVUMILIA HATA MWISHO NDIYE ATAKAYEOKOKA
Lk 12:35-40
Uvumilivu ni jambo la muhimu sana kuzingatia wakati huu wa siku za
mwisho.Uvumilivu ni hali ya kuwa na subira katika jambo fulani.Subira lazima
iambatane na matayarisho ili iweze kukaa.Matayarisho haya hufanyika kwa neno la
Mungu.Kazi ya hilo neno ni kukutia katika subira ulionayo.Maana si rahisi kuwa
na uvumilivu katika mengi ya dunia kama huna nguvu ya Mungu inayokuwezesha
kufanya hivyo.
Daudi alipakwa
mafuta akiwa na umri wa miaka 17, 1Sam 16:-12.Lakini ilimchukua miaka 13 hadi
alipokuwa mfalme wa Israeli 2Sam 5:4.Lakini utagundua kilichomfanya afanikiwe
ni uvumilivu uliokuwa ndani yake.Hata hivyo uvumilivu huo ulikuja kwa njia ya
Mungu mwenyewe maana haikuwa rahisi kwa Daudi kumuelewa Mungu ni kwa nini kama
alimtaka awe mfalme ampitishe kwenye shida nyingi ikiwepo kukimbizwa na Sauli
ikiwa moja wapo.
Hata ukimtazama
Ayubu unaweza ukajiuliza ni kitu gani kilimuwezesha akastahimili majaribu (Ayu
1:13-20) haya yote kwa kipindi kirefu.Cha kushangaza mara baada ya kupotelewa
na kila kitu aliishia kusema Bwana ametoa na yeye ametwaa jina lake lihimidiwe
Ayu 1:21-22.Kwa hali ya kibinadamu usingeweza kumuelewa bado.Wakati tunazidi
kujiuliza maswali mengi kwa nini aliweza tunapata jibu kuwa ni kwa sababu neno
la Mungu lilikuwa limemtawala ndani yake Ayu 1:9-10.
Wana wa Israeli
walipokuwa jangwani walipofika eneo ambalo walikosa maji waliingia katika
manung'uniko na lawama.Jambo hili lilimkwaza Mungu kwa sababu walikosa
uvumilivu Hes 14:11-21.Lakini baada ya ukosefu wa uvumilivu Mungu aliazimu
wasifike katika nchi ya Kanani Hes 14:22-24.
Nami sina hakika
kama Mungu amebadili uamuzi wake kwa watu wakosao uvumilivu katika maisha
haya.Basi tujiweke tayari maana hatujui ni wakati gani Mwana wa Adamu atakaporudi Mt 25:1-12
TUNASHINDWA
KUFANIKIWA KWA SABABU HATUMWAMINI MUNGU
Mt 20:29-34 Biblia
inatueleza habari ya vipofu wawili waliomlia Bwana Yesu awaponye mara tu baada
ya kusikia kuwa anapita. Hili lilikuwa jambo la imani kwao. Maana kwa kusikia
tu walipata kuamini Yesu anao uwezo wa kuwaponya Rum 10:17. Ndipo hata alipowauliza
awafanyie nini walijibu wanataka kupona. Nao walipokea kama walivyosema.
Utagundua
kilichowafanya waponywe ni imani ilikuwa ndani yao. Imani yao yaweza kuonekana
dhahiri pale hata waliponyamazishwa wao walipaza sauti zao wakisema "Mwana
wa Daudi uturehemu".
Watu wengi wanapoomba msaada kutoka kwa Mungu
ambao waweza kuwa uponyaji, ufaulu, kupandishwa kazi na mafanikio mengine
wanaposhindwa kupokea kwa mda waliotarajia wengi hukata tamaa na kuachana na
maombi na kuamua kufanya wanavyoona ya kuwa inafaa kwao. Hii hupelekea anguko
pasipo kujua kwao. Na kwa sababu hii hukutana na magumu sana hata wasiweze
kupata kabisa wanachokitazamia.
Natamani ukumbuke
kuwa wakati wale vipofu walipomwita Yesu awaponye walinyamazishwa hii ina maana
katika kuomba kwetu msaada wa kimungu kuna wakati msaada huo unacheleweshwa.
Tunapokata tamaa maana yake tunavunja makubaliano ya awali tuliowekeana na Mungu.
Hata kufanya ule msaada uliocheleweshwa kutofika kabisa.
Imani hukupa uhalali
wa kupokea kile unachokiomba. Lakini wengi wameshindwa kuamini hata kuwafanya
kukosa uhalali. Maana imani ni kitambulisho katika serikali ya Mungu impayo mtu
ruksa ya kuamua katika dawati la Mungu. Biblia inasema ijapokuwa alifanya ishara
nyingi lakini hawakumwamini Yn 12:37-43. Hivyo uwepo wa imani ya mtu
hausababishi na yeye kuitwa mkristo bali husababishwa na kusikia kwake Rum
10:17.
Wakristo wengi ni
wahudhuriaji wa kanisani lakini sio waamini. Hii hutokana na wao kufungwa na
mapokeo na sio neno la Mungu. Watu wengi hujishughulisha na mambo ambayo Mungu
hakuyaagiza ili wapate sifa na baraka ya watu. Hivyo kuwakosesha uhalali wa
umiliki kwa vile waviombavyo.
Maandalio ya moyo ni
ya mwanadamu bali jawabu la ulimi hutoka kwa Bwana ndivyo anavyotueleza
Mithali. Ina maana kama huna connection ya mbinguni katika vile uombavyo
haitakuwa rahisi kwako kuweza kupokea.
Ngoja nikueleze
ndugu yangu unayenifuatilia. Akuwaziayo Mungu siku zote ni yalio mema Yer
29:11. Tatizo linabaki kwako maana hayo akuwaziayo umeyakataa hivyo hana la
kufanya maana umeshindwa kuamini. Mwamini leo Yesu ili akupe ruhusa ya kuamua
na kupanga.
Ubarikiwe
Na Henry Nicholaus
JE UNAFAHAMU
UZURI WA MBINGUNI?
Mpendwa msomaji,
kwanza pole sana na shughuli nyingi za kila siku. Ninajua kwamba muda wako ni
mchache sana, kutokana na shughuli zako nyingi. Hata hivyo ninakuomba muda wako
mfupi tu, ili tuzungumze juu ya jambo muhimu ambalo nimeona kwanba ni vema nikushirikishe.
Je umekubali ombi langu? Natumaini umelikubali. Asante sana. Basi ninakusihi
tufuatane pamoja katika mazungumzo haya.
Huenda utakuwa
umewasikia watu wengi waliofiwa na ndugu, jamaa au marafiki zao wapendwa,
wakisema, ”Mungu waweke mahali pema peponi“. Jambo hili linadhihirisha jinsi
kila mmoja wetu anavyoamini kwamba kuna mahali pema peponi yaani mbinguni. Na
tena inaonyesha jinsi sisi sote na jamaa zetu tunavyopenda kwenda huko. Je,wewe
una shauku ya kwenda mahali pema peponi au mbinguni, baada ya kuiaga dunia hii?
Najua wewe pia una shauku ya kwenda mbinguni siku moja. Hata hivyo, shauku yako
itaongezeka zaidi utakapokuwa na ufahamu wa kutosha kuhusu uzuri wa mbinguni.
Peponi au mbinguni, ni wapi na kukoje? Peponi au mbinguni, kuna uzuri usioweza
kufananishwa. Tukifahamu jinsi mbinguni kulivyo kuzuri, kila mmoja wetu atazidi
kuwa na shauku ya kufika huko siku moja. Tufuatane basi ili upate ufahamu wa
kutosha kuhusu mbinguni au peponi.
Peponi au mbinguni
ni wapi na kukoje? Mbinguni au peponi, ni juu sana, mbingu ya tatu. Biblia
inasema katika 2 WAKORINTHO 12:2-4, ”Namjua mtu mmoja katika Kristo,…Mtu huyo
alinyakuliwa juu mpaka mbingu ya tatu. Nami namjua mtu huyo,…ya kuwa
alinyakuliwa mpaka Peponi…“ Mbingu ya tatu ni wapi? Mbingu ya kwanza, ni hii
iliyo na mawingu yanayoleta mvua, na mawingu mengine. Ni anga hili lililo juu
ambalo sehemu yake huonekana kwa macho ya kawaida. Ndege au eropleni zote
zinazobeba abiria, huruka katika mbingu hii ya kwanza. Mbingu ya pili, ni
mbingu iliyo mbali zaidi yenye sayari na nyota zote, Sayari zilizoko katika
mbingu ya pili, ni pamoja na Zebaki, Zuhura, Mars, Mshtarii, Zaharii, Uranus,
Neptune, na Pluto. Sayari nyingine ziko mbali sana. Kwa mfano, umbali wa dunia
yetu kutoka kwenye jua ni maili 93 milioni (kilometa 148,800,000). Lakini
umbali wa sayari ya pluto kutoka kwenye jua ni maili 3,666 milioni (karibu
kilometa 5,900 milioni). Nyota ziko nyingi sana, zinakisiwa kufikia bilioni
400. Nyota ziko mbali sana na dunia yetu. Nyota iliyo karibu zaidi na dunia,
iko karibu maili 26,000 bilioni (karibu kilometa 42,000 bilioni). Sasa basi,
baada ya sayari zote hizi na nyota hizi, ndiyo tunafika mbingu ya tatu. Mbingu
ya tatu, au Peponi, kwa msingi huu ni kilometa mabilioni kutoka hapa duniani.
Yesu Kristo alipopokelewa na wingu, na kupaa kwenda juu mbinguni ( MATENDO
1:9-11) alikwenda mbali sana kiasi hiki. Huko ndiko waliko watakatifu
waliotutangulia.
Tupige hatua tena na
kuangalia mambo mengine. Sasa je, mtu anapokufa, anasafirije kwenda mbinguni,
mbali kiasi hiki? Hatupaswi kuogopa kifo, ikiwa tunaishi maisha yaliyo mbali na
dhambi. Biblia inasema katika ZABURI 116:15, ”Ina thamani machoni pa Bwana,
mauti ya wacha Mungu wako“. Kufa kwa watakatifu ni faida (WAFILIPI 1:21). Ni
heri wafu wafao katika Bwana (UFUNUO WA YOHANA 14:13). Kufa kwa mtu anayeishi
maisha yaliyo mbali na dhambi, ni mwanzo tu wa utukufu. Mtu anayeishi maisha
yaliyo mbali na dhambi, anapokufa, roho yake humiminwa katika mwili mwingine wa
roho unaoitwa mwili wa mbinguni, kama mafuta yaliyo katika chombo kibovu
kinachovuja, yanavyoweza kumiminwa katika chombo kingine kilicho kizuri. Kufa,
ni kumiminwa! Mtume Paulo aliyepata neema ya kuchukuliwa na kupelekwa mpaka
mbingu ya tatu wakati wa uhai wake ( 2 WAKORITHO 12:2-4) ulipofika wakati wa
kufariki kwake, alijua ni wakati mzuri wa kumiminwa. Kwa maneno yake, katika 2
TIMOTHEO 4:6, alisema, ”Kwa maana, mimi sasa namiminwa, na wakati wa kufariki
kwangu umefika“.
Kuhusu miili ya
mbinguni, Biblia inasema katika 1WAKORINTHO 15:40-41,44, ”Tena kuna miili ya
mbinguni, na miili ya duniani, lakini fahari yake ile ya mbinguni ni mbali, na
fahari yake ile ya duniani ni mbali. Kuna fahari moja ya jua, na fahari
nyingine ya mwezi, na fahari nyingine ya nyota; maana iko tofauti ya fahari
hata kati ya nyota na nyota…Ikiwa uko mwili wa asili, na wa roho pia uko“.
Miili hii tuliyonayo ni mibaya sana. Ni kama vyombo vibovu. Fahari yake, yaani
uzuri wa ile miili ya mbinguni ni zaidi sana kuliko miili tuliyo nayo. Miili ya
mbinguni inang’aa mno na kupendeza sana. Mtakatifu anapokata roho, roho yake
mara moja humiminwa katika mwili mzuri wa jinsi hii. Mtu akiwa katika mwili wa
mbinguni, atapenda kujitazama wakati wote. Mwili huu hauna makovu wala ulema
wala makunyanzi ya uzee! Baada ya mtu kuwa na mwili mzuri wa jinsi hii, huvikwa
mavazi mazuri meupe sana yanayometameta sana. Weupe wa mavazi haya, ni weupe
usio na mfano duniani (UFUNUO WA YOHANA 3:4-5;7:9; MARKO 9:2-3). Baada ya
kuvikwa mavazi haya, mtu hufunguliwa mlango wa gari na malaika, na kuingizwa
katika gari zuri sana lisilokuwa na mfano duniani. Yako mabilioni ya magari ya
Mungu, yanayowasubiri watakatifu. Biblia inasema katika ZABURI 68:17, ”Magari
ya Mungu ni ishirini elfu, maelfu maelfu“. Mtu huchukuliwa na malaika katika
magari haya yanayoitwa magari ya moto, yanayoambatana na farasi wa moto na
kuchukuliwa kwenda mbinguni kwa upepo wa kisulisuli (LUKA 16:22; 2 WAFALME
2:11).
Magari yanayoitwa
magari ya kifahari yanayowabeba Marais na Wafalme duniani kama Mercedes Benz,
BMW n.k.si kitu yanapolinganishwa na magari haya. Magari ya Mungu hayatumii dizeli au petroli, bali huendeshwa
na upepo wa kisulisuli, na huenda kasi sana. Kwa muda mfupi sana, mtu hufika
mbinguni na kulakiwa na malaika wanaoimba nyimbo za shangwe. Hakuna mapokezi
yoyote ya Rais au mfalme yeyote duniani, yanayolingana na mapokezi ya mtu
anayeingia mbinguni, yanayofanywa na malaika.
Sasa tupige hatua
nyingine. Mbinguni kwenyewe kukoje? Mbinguni ni nchi iliyo bora kuliko nchi
yoyote duniani (WAEBRANIA 11:16). Waza juu ya nchi yoyote duniani inayowavutia
watalii wengi kutokana na uzuri wake. Nchi hii siyo kitu ikilinganishwa na
Peponi. Mbinguni ni kuzuri mno! Hakuna usiku wala mchana. Hakuna joto wala
baridi. Jua au mwezi havitumiki kutoa mwangaza. Utukufu wa Mungu ndiyo nuru ya
mbinguni (UFUNUO WA YOHANA 21:23-25). Neno ”Peponi“, linatokana na neno la
Kiyunani, ”Paradeisos“, linalotafsiriwa pia, ”Paradiso“, na kwa tafsiri fasaha,
lina maana ya ”bustani nzuri kubwa iliyojaa matunda mazuri“ na tena
linamaanisha mahali palipojaa furaha na raha kuu isiyo na kifani (UFUNUO WA
YOHANA 2:7; WAEBRANIA 4:1-11). Matunda ya miti iliyomo katika bustani hii
isiyokuwa na mfano, ni pamoja na mti wa
uzima uzaao matunda aina kumi na mbili. Maisha mbinguni, ni pamoja na kula
matunda haya katika bustani ya Mungu, na kupunga upepo wa raha kuu isiyo
kifani, Paradiso (UFUNUO WA YOHANA 2:7; ).
Kipi cha ziada tena
kuhusiana na mbinguni? Mbinguni, ni mji uliobuniwa na kujengwa na Mungu
(WAEBRANIA 11:10-16). Miji yote ya dunia hii imebuniwa na kujengwa na wanadamu
wenye upungufu wa ubunifu wa michoro, fedha, vifaa n.k. Mbinguni, ni mji
uliobuniwa na Mbunifu Mkuu, Mungu mwenyewe mwenye uwezo wote. Hakuna mji kama
huu duniani. Barabara zake siyo za lami, bali ni za dhahabu iliyo kama kioo
kiangavu ambayo hakuna mfano wake duniani. Mtu anapotembea barabarani, hujiona
kama katika kioo (UFUNUO WA YOHANA 21:21). Katika YOHANA 14:2, Yesu anasema,
katika mji huu kuna ”makao“ mengi. Neno la kiyunani linalotafsiriwa hapa ni
”mone“, linalotafsiriwa katika kiingereza ”Mansion“, katika Biblia ya tafsiri
ya King James Version. ”Mansion“, ni jumba kubwa la kifahari. Jumba la Meya wa
Jiji la London, Uingereza (”Lord Mayor of London), linaitwa ”Mansion House“.
Vivyo hivyo mbinguni, kuna makao mengi, au majumba mengi ya kifahari. Kila mtu atakayeingia mbinguni,
atapewa ”kao“, au ”jumba mojawapo la kifahari“, la kuishi. Kao lako
linakusubiri! Majumba haya, hayakujengwa kwa tofali za sementi au udongo, bali
kuta zake zimejengwa kwa madini ya aina nyingi. Biblia inasema katika UFUNUO WA
YOHANA 21:18-20, ”Na majenzi ya ule
ukuta wake yalikuwa yaspi, na mji ule ulikuwa wa dhahabu safi mfano wa kioo
safi. Na misingi ya ukuta wa mji ilikuwa imepambwa kwa vito vya thamani vya
kila namna. Msingi wa kwanza ulikuwa yaspi wa pili yakuti samawi; wa tatu
kalkedoni; wa nne zumaridi; wa tano sardoniki; wa sita akiki; wa saba
krisolith; wa nane zabarajadi; wa kenda (tisa) yakuti ya manjano; wa kumi
krisopraso, wa kumi na moja hiakintho; wa kumi na mbili amethisto“.
Vito hivi au madini
haya, yanafanya majumba ya mbinguni, yapendeze mno. Yaspi, ni madini
yanayong’ara sana yenye rangi ya kijani iliyochanganyika na bluu. Yakuti
samawi, ni mawe ya bluu, mazuri sana yenye ugumu unaofuatia madini ya almasi.
Kalkedoni, ni aina ya madini mazuri sana yenye rangi aina nne balimbali-nyekundu iliyochanganyika na njano,
hudhurungi (brown) iliyochanganyika na nyeusi, bluu iliyochanganyika na nyeupe,
na rangi ya maziwa. Zumaridi, ni madini yenye rangi ya damu. Krisolitho, ni
madini yaliyo kama dhahabu, ila yana rangi aina ya kijani iliyochanganyika na
njano, Zabarajadi, ni madini maangavu (yanayoona ndani), yenye rangi ya bluu iliyochanganyika na kijani.
Yakuti manjano, ni madini mazuri yenye
rangi ya njano na mchanganyiko wa kijani.Krisopraso, ni madini yenye rangi tatu pamoja; njano, kijani, na bluu.
Hiakintho, ni madini yenye rangi iliyochanganyika na njano. Amethisto, ni
madini yenye rangi ya zambarau, yenye bluu na wekundu ndani yake.
Nini zaidi? Mwangaza
wa mbinguni siyo kama wa duniani usio na rangi. Mwangaza wa mbinguni ni wa
rangi ya yaspi yaani kijani iliyochanganyika na bluu (UFUNUO 21:11). Mavazi
meupe ya wale walioko mbinguni, hubadilika
rangi mara kwa mara kutokana na rangi ya mwangaza na ya majengo hivyo
kufanya watu wapendeze mno. Ndani ya makao ya mbinguni kuna fenicha za
kifahari. Fenicha alizoagizwa Musa kuzitengeneza na kuziweka katika maskani,
zilikuwa mfano tu wa fenicha za mbinguni(WAEBRANIA 8:5; KUTOKA 25:9-40).
Chemchemi za maji na mito ya maji ya uzima inazunguka mji. Mbinguni kuna kula na kunywa, hakuna mauti wala maumivu au
taabu (LUKA 22:14-16, 29-30; UFUNUO 2:17; 21:4-5; 14:13). Kuna kuimba nyimbo za
sifa, na vinanda (UFUNUO 14:2-3; 15:2-4). Ufahamu wetu utaongezeka (1WAKORINTHO
13:12). Kuna mengi zaidi yasiyotamkika katika lugha hii ya duniani (WAKORINTHO
12:4). Ni heri twende wenyewe kujionea. Tusikubali mume au mke kutuzuia kuingia
mbinguni maana mbinguni hakuna kuoa au kuolewa (LUKA 20:34-36; MATHAYO
22:30).
Ni sifa ipi ya
kukuwezesha kuingia mbinguni? Ni utakatifu (WAEBRANIA 12:14). Ndani yake
hakitaingia chochote kilicho kinyonge (UFUNUO 21:27). Kinyonge ni kipi? Ni yule
anayetenda dhambi. Huyu ni mtu asiyefaa, Ni mnyonge! Je, wewe ni mtakatifu?
Jibu ni la! Maisha yako yamejaa dhambi, pamoja na kusema una dini, hivyo wewe
pia ni mnyonge, hufai kuingia mbinguni. Ukitubu leo dhambi zako zote kwa
kumaanisha kuziacha, na kuifuata njia ya Yesu Kristo, ndipo utakapopata rehema
ya kuingia mbinguni (MITHALI 28:13; YOHANA 14;6). Je, uko tayari kutubu sasa
ili upate rehema hii? Najua uko tayari. Basi fuatisha sala hii ya toba kwa
dhati kutoka moyoni,
”Mungu Baba, asante
kwa ujumbe huu. Hakika mimi ni mnyonge, mwenye dhambi. Sistahili kuingia
mbinguni. Natubu dhambi zangu zote kwa kumaanisha kuziacha. Kuanzia leo nataka
niifuate njia ya Yesu Kristo.Bwana yesu, niwezeshe. Asante kwa kunisikia katika
Jina la Yesu. Amen.“
Mpendwa msomaji
umekubaliwa kuingia mbinguni. Ili uzidi kudumu katika utakatifu mpaka siku ya
kuiaga dunia hii, hakikisha unahudhuria mafundisho katika Kanisa linalohubiri
wokovu. MUNGU AKUBARIKI!!!
UPO
UMUHIMU WA KUJUA NENO LA MUNGU
Biblia inatuambia Yesu Kristo ndiye Neno la Mungu.
Kwa maneno mengine Yesu ndiye Neno ambalo Mkristo anapaswa kuwa nalo (Yohana
1:1).
Kwa kusema hivyo
kuna umuhimu wa kumjua Yesu na kumshika,
kwa maana yeye ndiye Neno la Mungu. Katika Biblia mtume Petro anasema mbele za
Yesu kwamba, twende kwa nani na wewe ndio mwenye maneno ya uzima? Petro alijua
upo umuhimu wa kumjua Yesu kama Neno maana ndani ya Neno kuna uzima
Biblia inasema neno
la Kristo likae kwa wingi ndani yetu (Wakolosai 3:16).Kwa nini basi neno la
Kristo likae kwa wingi ndani yetu? Ni kwa sababu lina mambo yafuatayo ambayo ni
muhimu katika maisha yetu ya Ukristo. Mambo hayo ni…
A) Neno la Mungu li
Hai
B) Neno la Mungu
lina nguvu (Mwanzo 1:6).
C) Neno la Mungu
lina ukali kuliko upanga
D) Neno la Mungu
linachoma hata kuzigawanya nafsi, roho viungo na mafuta yaliyomo ndani yake
E) Neno la Mungu li
jepesi kuyatambua mawazo na makusudi ya moyo
KWA NINI NENO LA
MUNGU LI HAI?
Neno la Mungu li hai
kwa sababu Mungu mwenyewe
analithibitisha kwamba li hai maana
a) Linafanya
mabadiliko (Isaya 55:10-11).
b) Linatupa kushinda
dhambi (Zaburi 119:11).
c) Neno la
Mungu li hai kwa sababu linatupa
mafanikio katik mwili. Petro anasema ”kwa neno lako tunatupa nyavu zetu.“ Hapa tunaona kuwa Neno la Mungu pekee yake ndilo linaloweza kuleta majibu
katika maisha yetu (Luka 5:3-6).
Uhai wa Neno la
Mungu kwa mtu ndio unaoleta kushinda dhambi. Nao wakamshinda kwa neno la
ushuhuda wao (Ufunuo 12:11).Daudi aligundua au kwa maneno mengine alifahamu
umuhimu wa neno la Mungu katika maisha, kama vile mtume Paulo anavyosema na
Wakolosai kwa habari ya neno la Kristo kwamba likae kwa wingi ndani ya mioyo
yetu
Neno la Mungu lina
nguvu na ndio maana tunamshinda shetani kwa neno la Mungu.Yesu kama kielelezo
yeye mwenyewe ni neno ndani ya neno anamshinda shetani (Luka 4:1-12).
Katika mistari hiyo
tunaona Yesu anamwambia shetani ”imeandikwa“
Shetani nae anageuza usemi nae anamwambia Yesu ”imeandikwa kwamba atakuagizia
malaika usije ukajikwaa mguu wako.“ Kwa kuwaYesu neno la Mungu limo ndani yake
hamwambii tena shetani imeandikwa ila anamwambia imenenwa. Kwa maneno mengine
tukiwa na neno la Yesu ndani yetu hatuwezi kuyumbishwa. Kwanini? Kwa sababu
tumeshaona jinsi ambavyo shetani
anajaribu kutumia neno la Mungu
kwa kusema ”imeandikwa.“ Na ni
kweli imeandikwa ananukuu kutoka kitabu cha Zaburi 91 :1-12. Hata kama shetani
ananukuu maandiko haina sababu yamimi
kushindwa na shetani maana Yesu tayari
alikwisha mshinda. Yesu kumshinda shetani ina nipelekea mimi kusoma neno la
Mungu kwa bidii sana. Kwa mfano, ni kweli kabisa imeandikwa mtakula vitu vya
kufisha havitawadhuru lakini je, ninywe sumu sitakufa kwa sababu imeandikwa?
Hapana, ukinywa hakika utakufa. Shetani hutumia mandiko kuwafunga wasiojua neno
la Kristo Yesu.
Katika Biblia
tunasoma pia kwamba ”imeandikwa“ Wanandoa MKE na MUME wasinyimane. Kwa kutojua
neno vijana wa kiume na wa kike wamedanganywa. Si hao tu hata walioko kwenye
ndoa wametegwa kwa andiko hilo. Neno linasema katika Mithali 6:32 ”Aziniye na
mwanamke hana akili kabisa“ na Mwanamke vivyo hivyo akizini na mwanaume hana
akili kabisa. Watu wamepata hasara ya mambo mengi kwa kutojua neno la Mungu.
Ili tuweze kumshinda shetani ni lazima neno la Yesu liwe ndani yetu ndiposa tutamshinda shetani. Ayubu kwa
neno la Mungu alishinda. (Ayubu 19:25-27, Waefeso 6:17).
Nataka nikwambie
neno la Mungu ni msaada katika maisha yetu maana hutupa majibu ya maisha yetu. Katika Luka 5:3-6
tunasoma jinsi Petro na wenzake walivyopata samaki wengi kwa kutii neno la
Kristo. Kumbuka pia juu ya yule akida, alimwambia Yesu ”...sema neno tu na
mtumwa wangu atapona“ (Luka 7:2-10). Yesu akisema neno lazima mabadiliko
yatokee. Neno la Mungu lina ukali kuliko upanga. Kwa nini neno la Mungu lina ukali kuliko upanga? Upanga unaweza
kukukata na usipone. Lakini neno linakata na kuponya. Kwa neno hili wafalme
wanatubu. Yona alitumia neno la Mungu likawa kali watu wakatubu. (Yona 3:1-10;
Matendo ya Mitume 8:18-24).
Neno la Mungu
linachoma hata kuzigawa nafsi na roho na viungo na mafuta yaliyomo ndani yake
(Matendo 7:51-54, Yohana 4:16 -18, 27-29). Mwanamke akaambiwa mambo yake; Neno
likachambua kila tabia. Neno la Mungu li jepesi kutambua mawazo na makusudi ya
moyo.Yesu kama Neno la Mungu anajua mambo ambayo watu wanawaza ndani ya mioyo
yao (Luka 5:17-24, 6:6-8 ; Mathayo 16:1-4). Yapo makusudi ya moyo ambayo ni ya
siri sana kwa mwanadamu lakini nataka nikuambie neno la Mungu ni jepesi kutambua makusudi ya moyo.
Mtume Petro
aliyependa kujua neno la Mungu, naye pia Mungu alimjalia neema ya kuyajua
makusudi ya moyo wa mwanadamu (Matendo 5:1-11). Elisha aliyajua makusudi ya
moyo wa mfalme ya kuwatenda Israeli kwa siri ila Mungu alimpa neema ya kuyajua
mawazo ya mfalme (2 Wafalme 6:8-12). Hili ni jambo la msingi katika maisha ya
Mkristo yaani kulijua neno la Mungu. Neno la Mungu tukiwa nalo na likitenda kazi ndani yetu
lazima tufanikiwe (Yoshua 1:8) .
Je unahitaji kuwa na
imani katika neno la Mungu? Basi, ni neno la Mungu peke yake ambalo laweza
kuumba imani, maana pasipo neno la Mungu hakuna imani (Waebrania 11:3 ;
Warumi10:17). Ili uwe mwanafunzi wa Yesu ni lazima ulijue neno la Mungu na
kulishika.(Yohana 8:31 ; Luka 2:19). Kama neno halimo ndani yetu tunayoyafanya
yanakuwa hayana Mungu, hata twaweza kusalitiana. Mtu anayelitamani neno la
Yesu huling’ang’ania na kulitenda maana
kwake ni nguvu. (1Wakorintho 1:18). Si kwamba Neno la Mungu ni nguvu tu: bali
huleta faida (Mathayo 13:23).
Watu wengi tunapotea
kwa kutokujua uwezo (nguvu) iliyomo katika neno la Mungu (Mathayo 22:29).Yesu
anasema, mtu anayelitenda neno la Mungu na kulishika huyo amepanda mbegu ambayo
itazaa sana, maana ndani ya moyo wake imo mbegu ambayo ni neno la Mungu la uponyaji
na mafanikio, msamaha, utu wema na mengi yanayofanana na hayo.
Yapaswa maisha yetu
yawe yenye neno (mbegu) la Mungu ili
tuweze kuzaa mambo mazuri. Wokovu wetu unaimarika kwenye neno la Mungu. Hilo
neno la Mungu tunalipata wapi? Isaya 34:16. Upo umuhimu wa kuyachunguza
maandiko ili kujua Mungu anasema nini (Matendo 17.10-11). Je, tangu ulipowekwa msingi wa wokovu, neno
limo ndani? (Hagai 2:18-19). Kila kitu kinaweza kupita lakini sio neno la Mungu
(Isaya 40:8, Mathayo 24:35).
Ili neno litende kazi katika kinywa chako
unapolitamka na kuamini ni lazima iwepo nguvu ya Roho Mtakatifu. Bila hii nguvu
hamna kitakacho endelea. Utasema umeamini lakini hakutakuwa na matokeo. Mungu
mwenyewe alipotamka neno liliambatana na nguvu ya Roho Mtakatifu (Mwanzo1:2-3).
MAISHA
TULIONAYO LEO YANA NAFASI YA KUBARIKI AMA KULAANI VIZAZI VIJAVYO
2Fal 4:1-7
Inatueleza juu ya mwanamke mmoja ambaye alikuwa amefiwa na mumewe ambaye
alikuwa mwana wa nabii.Mumewe alikuwa anadaiwa na hata alipofariki hakuwa
amelipa hilo deni.Hivyo kumfanya yule aliokuwa anamdai kutaka kuwachukua watoto
wa yule mama na kuwafanya kuwa watumwa
kama malipo ya hilo deni.Jambo hili halikumpendeza yule mama na kuamua
kumwomba Elisha amsaidie tu kwa sababu mumewe alikuwa mcha Mungu.
Hivyo utaona yule
mama aliomba msaada kwa Elisha kwa sababu kuwa mumewe alikuwa mcha Bwana na
Elisha aliamua kumsaidia.Hivyo kigezo cha Mungu kumsaidia yule mama kupitia
Elisha ni kwa sababu mume alikuwa ni mcha Mungu.Maana yake Mungu ana utaratibu
wa kuachilia msaada kwa watu kwa sababu ya wazazi wao au ndugu zao au waume au
wake zao walikuwa wanamtukuza.
Hili utaliona kwa
Ibrahimu ambaye Mungu alibariki vizazi vyake kwa sababu tu ya maisha ya
kupendeza aliokuwa nayo mbele zake katika maisha yake Mw 17:4-7.Ukiona familia
au ukoo fulani umebarikiwa uwe na uhakika kuwa ni kazi nzuri iliofanywa na
baadhi ya watu waliopita katika familia hiyo au ukoo uo ambao ulimpendeza
Bwana.Na kwa sababu hiyo akaamua kuwa bariki kupitia maisha ya hao.
Hata hivyo maisha
mabaya ya mtu huweza kusababisha shida kwa vizazi vyake kama isemavyo Hes 14:18
Mungu huwapatiliza wana wa uovu wa baba zao katika kizazi cha tatu na cha
nne.Hivyo basi mkao mbaya tuliokuwa nao leo huweza kusababisha maisha mabovu na
ya shida kwa vizazi vingine.Maana siamini kama Mungu amebadili utaratibu huu
hata leo.Mungu ana taratibu mbalimbali ambazo amejiwekea katika ulimwengu wa
roho kama ulivyo utaratibu wa mzaliwa wa kwanza.Na utaratibu mmoja wapo ni huu
wa kubariki watu sawa na mikao mizuri wa mababa zao na kulaani pia sawa na
mikao mibaya ya mababa zao.
Najua uliwahi
kusikia mtu akisema kuwa anasumbuliwa na magonjwa ya kurithi kama pumu.Uliwahi
kujiuliza kwa nini iwe magonjwa ya kurithi?Hii ni kwa sababu yamkini yuko mmoja
ambaye hakukaa vizuri hata kuweza kusababisha laana ya magonjwa kutafuna ukoo
wao.Kama nilivyokueleza uko utaratibu ambao alijiwekea Mungu hivyo Mungu
huangalia huo katika kuamua vitu mbalimbali.
Hivyo kaka
yangu,dada yangu,baba yangu na mama yangu kumbuka Mungu hukuazia mema siku zote
Yer 29:11.Hivyo chagua mkao mzuri ili ujenge msingi mzuri wa kizazi chako
kijacho.Kumbuka itakuwa jambo la furaha kama vizazi vyako vikifanikiwa kwa
sababu yako.
Ubarikiwe
Na Henry Nicholaus
THE HOLY
SPIRIT WORKS
Before Jesus Christ
descends to heaven, he said that we his people shall be sent a helper who will
assist us in everything after he has left. The helper or our assistant is the
holy spirit. The holy spirit was sent to us in so many things in our daily life
of today. The holy spirit make sure that we are able to make the right decision
that is to please God. God wants everyone to obey his commandments because if
one lives in them, he/she will never
commit a sin.
Satan does not like
it when a person pleases God because he does not want to be the only one who
will end up in the everlasting fire, so he tries to make everyone go against
what God wants so as the person to be punished by God to the everlasting fire
with him.
The Work of the Holy Spirit
When Satan keeps
temptations on a God's child, the holy spirit is the one who prevents and help
the child to overcome the temptation and trials from Satan. The holy spirit is
the one who gives ways to an individual so as to live a life that will always please
God.
Remember when you
had feeling when you were alone at your dining table that you should take your
fellow's bread early in the morning then
there is this part of you inside was telling you that, "Just take it and
eat, you are very hungry now and by the way the owner of the bread will take
break some few minutes and hours from now". But there is also this part in
you which was telling you that, "What you are about to do is very wrong,
because the owner of that bread is also hungry and also what is yours is that
what you have been kept for only. If you take it, you will hurt the
owner". The one telling you this is the holy spirit but the first sound
was Satan.
Satan will always
want to make you do the wrong things but the Holy Spirit will always lead you
to the right path and that part is God's. The Holy Spirit will not lead you to
hurt somebody or being disobedient to God. In your life you will always hear these
two sounds. That is the bad one and the good one. Be able to differentiate them
because the bad one is Satan's and you will always hear it telling you to do
something against God's will. Always choose to listen to the good one because
that is the Holy Spirit talking to you. The Holy Spirit will always tell you to
do God's will.
Where the Holy Spirit Dwells
Everyone has got the
Holy Spirit in him or her but it depends on how each one allows the Holy Spirit
to operate. The holy Spirit does not dwell in an unpleasant soul in front of
God. This tells us that we should always please God and make our souls clean
because a clean soul is the temple of the Holy Spirit 1Cor 3:16
Question : How do we please God?
Answer
: We please God by doing all that he wants us to do that is to obey and
follow his commandments. For all those who go against God's
commandments in which does not please God, the Holy Spirit does not dwell in
them. Always pray for the Holy Spirit to dwell in your and most of all prepare
a good environment for him to live in that is a good temple.
This temple is
nothing else but your body. Treasure your body, keep it free and clean from all
Satan's dirt. Respect your body and keep it the way God wants you to keep it as
a Christian. If you do all this your body will always be the temple of the Holy
Spirit and he will dwell in you.
How to Make the Holy Spirit Work/Operate in you
Always pray :Prayers are very powerful, if you
did not know this you should know it by now. Prayers connect you with God. The more you pray,
the more the Holy Spirit gets the chance to operate in you. This tells us that
by our prayers is when the holy spirit works in us.
Read the word of God: The word of God is the
food of our souls. When we feed our souls with God's word, the Holy Spirit
dwells in us and operates and we even get the chance to know him well and how
to use him in our daily life.
Do not commit sins :When one commits a sin, he
or she chases away the Holy Spirit because the Holy Spirit never operates in a
dirty soul. Ask the Holy spirit to give you the strength and ability to
overcome all Satan's and trials and he will do so.
Respect your body :Your body is the temple of
the Holy Spirit. If you impurify it ,example wearing improper clothes, sex out
of wedlock or before marriage then you are going to chase the Holy Spirit away.
When one faces
hardship in life or in a dilemma such that he or she does not know what to do,
he or she should ask the Holy Spirit to show him the way out of it or to know
on which path he or she should take. No matter how hard the problem is or how
much complicated it is one should just call for the Holy Spirit's help and he
or she will get a way out (solution). There is nothing which is impossible to
God therefore one should know that there is a solution to everything.
A Christian's life
is not always straight. There are always temptations and trials that he or she
will face. They are always there so as God can know how much faith that one has
and also they are a part of Satan so as to get followers. In order to overcome
them, one should ask the Holy Spirit to always lead or direct him or her in the
paths that will make him or her out/through it and will make him or her meet up
with God in the end.
If one's faith is
very strong, the Holy Spirit may lead him or her speak in tongues. Speaking in
tongues is led by the Holy Spirit and it is the language spoken in the world of
faith. This language works and Satan cannot interfere with it. In order one to
have such a capability, he or she should pray hard for the Holy Spirit to help
him or her to have it. One does not get it easily because it can also not be
forged. The Holy Spirit controls everything in this.
If you feel the Holy
Spirit wants to talk to you or to work in you in anyhow, do not stop him. The
word of God says that if one tries to do so then he or she is committing a sin.
Everyone must have the Holy Spirit in him or her because in the absence of the
Holy Spirit one will always commit sins and he or she will end up in the
everlasting fire.
At this time, Satan
is hunting really hard for souls that will go with him to hell, therefore we
should pray very hard for the Holy Spirit to dwell in us and give him our lives
so as he can control and operate them and in the end, we go up in heaven and have
an everlasting happy life with Christ the Lord.
Be blessed
By Margret
Ng'ondia
NI VIGEZO
GANI TUVITUMIE WAKATI WA KUOMBA?
"Na
huu ndio ujasiri tulio nao kwake, ya kuwa, tukomba kitu sawa na mapenzi yake,
atusikia". 1Yoh 4:14
Maombi
ni mawasiliano kati ya Mungu aliye hai na mwanadamu. Utaratibu huu haukuwepo
awali bali ulikuja mara baada ya dhambi kuingia duniani ikumbukwe kuwa wakati
wa mwanzo wa misingi ya dunia Mungu alikuwa akimtembelea Adamu na kuongea naye
hivyo maombi hayakufanya kazi maana Mungu alikuwa karibu mno na mwanadamu Mw
3:8-10 utaona ndio utaratibu kuwa tembelea Adamu na Hawa.
Hivyo
basi mara baada ya dhambi kuingia ilimsogeza mwanadamu mbali na uso wa Mungu
hivyo kupelekea uwepo wa mawasiliano mapya yanayohitaji imani ili yafanikiwe
maana pale mwanzo imani haikuwa na nafasi maana Adamu alimwona Mungu. Hivi sasa
uko umuhimu wa imani maana Mungu haonekani kwa jinsi ya mwili. Imani ni kuwa na
uhakika ya mambo yatarajiwayo ni bayana ya mambo yasiyoonekana kama isemavyo
Ebr 11:1. Katika maombi imani hukupa uhalali wa kuweza kupokea kile
tukiombacho.
Imani
hiyo humwakishishia Mungu huyu ndiye sahihi mpe maana astahili, lakini licha ya
uhakikisho huo sio kigezo pekee kitufanyacho yale tumwombayo Bwana basi tuweze
kupokea. Kigezo kingine ni kuomba sawasawa na mapenzi ya Mungu. Sawa imani
inakupa nafasi ya kuweza kupiga simu mbinguni hio ni hatua moja lakini kupokewa
ni hatua nyingine na kujibiwa ni jambo jingine pia. Natamani tutazame maombi
kwa mtazamo wa hili Roho Mtakatifu analokufundisha wakati huu. Naomba usichoke
kukaa naye maana kuna vizuri anavyotamani akufundishe kwa ajili ya afya yako
wewe na wengine pia.
Paulo
mtume alisema mna omba lakini hampokei kwa sababu hamwombi sawasawa na mapenzi
ya Mungu. Kuomba huko ni kwa namna gani? Huku ni kuomba kwa msaada wa Roho
Mtakatifu. Unajua yamkini yako mambo mengi ya kuombea ila namna yakupeleka
mbele za inaweza ikawa kikwazo hivyo unapomshirikisha Roho Mtakatifu yeye
hukupa usemi sahihi na maeneo gani tusimame.
Ngoja
nikueleze kuomba kwa Roho Mtakatifu ni kwa ajabu sana maana licha ya wewe kuta
kuombea vitu vyako lakini anakupa msukumo wa kuombea vitu vingine ili Mungu
apate kuingilia mahitaji yako. Hata hivyo unaweza ukany'any'ania kuombea mambo
yako na kumbe kuna 'barrier' inayokuzuia kujikonecti na madhabahu ya Mungu
hivyo kuomba sawasawa na mapenzi ya Mungu ni kuomba kwa utaratibu kwa msaada wa
Roho Mtakatifu.
Unaposoma
Yn 16:24 inasema Hata sasa hamkuomba neno kwa jina langu; ombeni, nanyi
mtapewa; furaha yenu iwe timilifu. Unaweza kuwa na furaha kila wakati maana
ndio biblia ituambiavyo Fil 4:4 Hivyo basi utaona kuwa furaha tunayo lakini sio
timilifu. Utimilifu wake huja pale tupokeapo vile tuviambapo. Hivyo yatatimia
hayo kama ukiweza kuomba sawasawa na mapenzi ya Mungu. Mungu akutie nguvu
katika hili ewe mpendwa ulie ichagua huduma hii.
Barikiwa
sana
Na
Henry Nicholaus
KUNA MAENEO
AMBAYO TUMEFUNGWA NA NDIO MAANA HATUFANIKIWI
"Na sasa,
tazama,nakufungulia leo minyororo hii iliyo mikononi mwako…" Yer 40:4
Watu wengi huweka
mikakati mingi wapo anza mwaka mfano kama tulivyo anza 2013. Lakini mara nyingi
anapomaliza mwaka anagundua kuwa katika mikakati mingi aliojiwekea baadhi yake
tu ndio iliyofanikiwa. Hii husababishwa na minyororo ambayo imewafunga watu katika
maisha yao. Ndio maana Mungu anatueleza habari za kuwekwa huru katika mstari
unaotuongoza hapo juu.
Efe 1: 3 Biblia
inatueleza kuwa tumebarikiwa na Mungu baraka zote za rohoni. Ina maana gani?
Mungu amekupa kibali katika kila lengo lililojema katika maisha yako. Lakini
minyororo ndio imekuwa kikwazo katika kufanikiwa ndio maana hatuoni udhihirisho
wa baraka hizo.
Dhambi kama moja ya
mnyororo ambao umewafunga wengi ndio umekuwa mnyororo unaotesa wengi. Kwa
sababu wengi waipenda dunia na biblia inasema ukiipenda dunia kumpenda Mungu
hakupo ndani yako. Tunapotazama 1Kor 3:16 tunaona kuwa miili yetu ni hekalu la
Mungu. Kwa maana hiyo tunapotenda dhambi tunamzuia Roho Mtakatifu kukaa ndani
yetu hivyo tutakayo yaamua na kuyapanga yatakuwa yamekosa kibali cha Mungu.
Hivyo kupelekea kutofanikiwa kwa mambo yetu Mith 16:1. Hata ukisoma Rum 3:23
biblia inasema kwa kufanya dhambi tumepungikiwa na utukufu wa Mungu. Ukosefu wa
utukufu wa Mungu wakati wa kufanya maamuzi huathiri matokeo ya baadae.
Hata hivyo imani
nayo ni mnyororo mwingine ambao umekuwa kikwazo katika mafanikio. Wengi hawana
Imani katika wanayotazamia kufanya au wayaombayo. Hivyo kusababisha anguko lao.
Imani ni kuwa na hakika ya mambo yatarajiwayo Ebr 11:1 hivyo basi unapokosa uhakika
kwa kile ulichoazimia ulipoanza mwaka hauwezi kufanikiwa. Imani hukupa uhalali
wa kupokea kile ambacho kwa hali ya mwili hakipo kwa wakati huu. Pasipo kuwa na
imani hatuwezi kuomba maana ni sawa na kazi bure.
Sadaka pia
husababisha watu kutofanikiwa kama isipotolewa kwa uaminifu Mal 3:10 Biblia
inasema tupeleke chakula ghalani mwa Bwana naye atatufungulia madirisha ya
mbinguni. Tunapopokea hukumbuki kutoa tukisahau kama sisi nasi pia tumepokea
kutoka kwa Mungu. Wengi huona wamepata kwa nguvu zao kisa waliangaika na kupata
fedha. Lakini Mungu ndie aliefanikisha mchakato wote. Sadaka ni moja ya eneo
linalomgusa sana Mungu. Ukisoma hata Elia alitumia kigezo hiki kuweza
kumdhirisha Mungu wa kweli kati manabii wa baali.
Hivyo ni vyema
unapoanza mwaka 2014 usitamani kufanya makosa tena. Tazama hiyo minyororo kisha
amua kubadilika ngoja nikueleze huna hasara kama utaamua kubadika. Kumbuka
mabadiliko haya yatakufanya utofautiane na wengine katika mtazamo na mwenendo
hilo lisikuogopeshe bali tamani mafanikio tu achana na wanadamu kwa maana hao
siku zote wapo. Hata hivyo biblia inatuonya tukiipenda dunia kumpenda Mungu
hakumo ndani yetu.
THE WORD OF
GOD
The word of God is
power and the power is transferred to one place by the means of prayer through
faith in the name of Jesus Christ. We pray for people to transfer the power of
God's word that brings healing, deliverance and blessing. A servant has a word
of God from God. The word God brings changes by its power that is working by
prayers from faith. It is from that one can receive the power of God's word to
change salvation.
The word of God must
be spoken to anything, the word of God is spirit which gives life to anything
hearing the word of God. That why if we speak to dry bones will set life spirit
of darkness will flee away and presence of God to reign from Holy Spirit. By
God's word we can speak to anything even that which has no life to have life
because God speak to the lifeless and change them to abundant life the void
face of the that has no form.
We need to pray so
that Holy Spirit can make us to speak the word of God and so that we may speak
by his authority of the Holy Spirit. Changes required by the word of in life of
people. This is why God gives us his word. It is important to receive the word
of God because it changes everything as we learn to speak by the authority of
the Holy Ghost. We seek this in prayers to ask the Holy Spirit to make us bold
to speak the word of God.
Speak from the Holy
Spirit
When we speak the
word of God the power in the word of God is released and brings effects and to
speak by the help of Holy Spirit in this. Without the power of the Holy Spirit
we are not strong enough to speak the word of God as it is needed. Many time in
our lives are still the same because we have not understand to make the word of
God real. It must be spoken by the tension and be heard. We need to understand
how Holy Spirit will use our mouth to speak the word of God.
Holy Spirit speaks
through us. He makes the will of God to us by speaking the word of God. We say
healing but don't see healing, we say blessing no blessing, we say A no A , we
say prosperity, we rebuke, we destiny works of the evil are still see nothing.
Let the one inside you speak through you. This is the problem to many. Many
people don't let the Holy Spirit speak through them by this don't give a room
to Holy Spirit to speak the word through them.
God has promised
whatever we need in his word in John 14:16. If you love me you will obey my
command and I will ask my father to give
you a counselor who will be with you forever. Also in John 7:31 whosoever
believes in me as the scripture has said streams of the living water will flow
within him and by this he meant the spirit.
Holy Spirit (help us
to speak the word through us. Believe in the name of Jesus. This is the command
of God. And those who believe the following signs they will speak in tongue put
hands in the sick and get health. Speaking in tongues is very important in
this. John 6:6 The words which Holy Spirit speak to you are spirit. If you are
in Christ you possess promise victory. You don't need to ask for it . When you
in Christ the bible says you are not condemned but your are righteousness you
have all the promise of God to you as his child he says you are the heir
according to the promise of God. Don't think God is going to bring them no you
have right in them. You have power anointing victory and all that he promised
as the child of God to have, you just need to believe to have them. God has
given us in the spirit and receive them in the spirit as use them by the spirit
for the good of God. You have all first chance between for what you have with
rejoice heart. I have it through faith in Christ Jesus.
When you are in
Christ, victory is yours because God has promised victory to his children not
other else and if you are a child of God the promise is fulfilled in you. I
just need to say I have it Satan cannot take it from me because I have been
made righteous by the blood of Jesus. What Satan tries always because he is not
able to take what belongs to you by fear. Fear makes you lose your right as a
child of God . When fear comes just tell Satan and am a child of God it is
over. He understands and leaves. Because the word says you did not receive the
spirit of fear but of son ship. Then if and am a son of God am the heir of his
promise. If am a child of God the spirit of fear cannot dwell in me. Then fear
goes away from my life because it is the same word that chased him, I will say
again and again. Amen and Amen to my Soul.
Be blessed
By James Nyimbo.
UPATANISHO
TENA
Unaweza kuanza
kuwaza kwa nini neno upatanisho tena na
sio upatanisho hilo lisikupe shida bali andamana nami wakati huu ili uweze
kuelewa nini makusudi ya Mungun katika hili.
"Watu wale
waliokwenda katika giza wameona nuru; Wale waliokaa kwenye uvuli wa mauti nuru
imewaangaza, Umeliongeza taifa, umezidisha furaha yao; Wanafurahi mbele
zako,Kama furaha ya wakati wa mavuno, Kama watu wafurahiyavyo wagawanyapo
nyara. Isa 9:2-3
Kwa muda mrefu
tulitembea katika shida kubwa kwa kutangatanga na katika giza totoro. Lakini
Mungu akiona hili aliamua kumwachilia mwanae mpendwa Yesu Kristo ili arudishe
furaha tena. Hivyo Yesu alikuja kwetu kama kipatanisho kati ya mwanadamu na
Mungu aliye hai.
Kwa nini
kutupatanisha tena? Ukumbuke kuwa toka mwanzo mwanadamu alikuwa rafiki wa
Mungu. Mara ya dhambi kuingia katika bustani ya Edeni jambo hili lilisababisha
mawasiliano ya Mungu na mwanadamu kuwa magumu. Kwa sababu Mungu hakai karibu na
dhambi hivyo ile hali ya Adamu kutolewa katika bustani ilikuwa na maana yake
yaani kuvunjika kwa mawasiliano ya karibu na Mungu.
Mara baada ya
kuvunjika mawasiliano hayo maisha ya mwanadamu yakawa ya miangaiko mingi hivyo
atakaye jitaabisha ndiye atakaye kula asiyefanya hivyo atakaa na njaa. Yesu
anakuja kuleta neema kwa njia ya Mungu ili tuwe na Mungu tangu ile zamani Yn
3:16.
Unajua dhambi ni
kitu kibaya sana ilisababisha mwanadamu apoteze nafasi aliokuwa nayo ya
kumiliki na kutawala ipotee. Na nafasi hiyo kuchukuliwa na shetani basi ujio wa
Yesu ulikuwa wa thamani sana kurudisha nafasi ya mwanadamu mbinguni na duniani.
Unaposoma Mt 16:17-19 Yesu anamweleza Petro kuwa amempa funguo za ufalme wa
mbinguni atakalolifunga duniani na mbinguni litafunguliwa atakalolifungua
duniani na mbinguni litafunguliwa. Kwa utaona kwa ujio wa Yesu nafasi yetu ya
utawala na kumiliki imerudishwa. Ndio maana kusema nimekupa funguo za ufalme wa
mbinguni.
Upatanisho huu haupo
kwa mtu ambaye hamwamini na kumkubali Yesu kama asemavyo Yn 1:11-12
"Alikuja kwake,wala walio wake hawakumpokea. Bali wote waliompokea aliwapa
uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake". Maana
wako wengine wanamchukulia Yesu kama wa kawaida kumbe sivyo hawa wote na
wengine wakataao kuwa yeye si Mungu hili jambo haliko kwao.
Hivyo kwa upatanisho
wa pili ndugu mpendwa tumebariiwa kwa baraka za rohoni kama asemavyo Efe 1: 2
.Si tu hilo tumechaguliwa na yeye na kuwekwa muhuri na Roho Mtakatifu hili ni
jambo la thamani kwetu hususani ukitazama kuwa yeye Roho wa kweli hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa Rum
8:26 hili ni la thamani sana.
Kuzaliwa kwa Bwana
Yesu ni neema na baraka kwa wengi hususani wale waeleao maana yake. Kwa sababu
amekuja lakini sio wote wanaona sababu ya kumkabidhi maisha yao. Wewe ambaye
umefahamu hili kwa msaada wa Roho wa kweli nenda ukafanyie kazi jambo hili maana
hutajuta hata siku moja kwa busura unayochukua leo. Nakushukuru sana maana
umemsikia Mungu. Basi sema sala hii
Baba wa Mbinguni
uliye umba vyote nakushukuru kwa pendo lako lisilo na kipimo kwetu. Asante
maana umekubali nirejee kwako tena. Nakusihi usitazama zamani zangu mbaya bali
unirehemu kama neno lako lilivyonifundisha kwa habari ya upatanisho. Asante kwa
kuwa unanisikia, sifa na heshima ni vyako. Amen.
Na Henry Nicholaus
Barikiwa sana.
KUNA
MAHUSIANO MAKUBWA KATI YA KUTOA SADAKA NA MAJIBU YA MAOMBI YAKO
Utoaji wa sadaka
unafananishwa na upandaji wa mbegu. Kanuni ya kutoa sadaka inafanana na kanuni
ya kupanda mbegu shambani. Mkulima timamu lazima atajiuliza kuwa nitaandaa
shamba halafu nitapanda mbegu kwa kiasi kipi? Na mbolea gani atatumia na kwa
kiasi gani? Na atavuna nini kwa kiasi gani na kwa ajili ya nini? Wengine
kusomesha watoto, kununua gari, nyumba, kupata mtaji mwingine.
1Fal 18:21-29 Mungu
hujidhihirisha kwa sadaka. Elia alikuwa
na mabishano ya kidini na manabii wa mabaali, hivyo akawaambia wanunue ng'ombe
wawili na kisha watoe sadaka Mungu atakayejibu kwa moto huyo ndiye mungu wa kweli.
Biblia inatuambia Elia aliwaambia waanze wao, waliangaika hadi kujichanja miili
yao lakini hakuna kilichotokea hivyo ikawa zamu ya Elia naye akawaambia wamwage
maji juu yake lakini Elia alipoomba moto ulishuka kutoka mbinguni na kuchukua
sadaka.
Swali : Unadhani ni
kwa nini mungu wa baali alishindwa kushuka?
Jibu : Hii ni kwa
sababu Mungu wetu anapowekewa sadaka hataki ushirika na mtu hivyo basi. Miungu
mingine lazima ikae pembeni wakati ambao Mungu anashuka maana hakuna
kinachoweza kustahimili nguvu yake. Ndio maana miungu mingine ilikaa kimya.
Mungu anapotamani
kusema na wewe usikatae. Maana kuna neema ambayo inataka kushuka ndani yako.
Inawezekana hukumwona Mungu kwa macho ya damu na nyama. Lakini ndio staili ya
Mungu kushuka katika sadaka. Kila sadaka inatakiwa kuwa na ujumbe nyuma yake
2Nya 1:1-10. Wakina dada msikubali ofa za ovyo maana hata ofa nazo zinaujumbe
nyuma yake uliofichika. Suleimani baada ya kutoa sadaka ya kuteketeza ya
maelfu. Mungu akashuka akamwambia na ujumbe sasa ni nini?
Unapoitazama sadaka
itazame kama mkulima maana yeye huwaza mavuno kwa lengo kuwa atavuna kiasi gani
na kwa ukubwa gani? Ebr 11:4 Habili alitoa sadaka kwa imani. Imani ni kuwa na
hakika ya mambo yatarajiwayo. Habili wakati
anatoa sadaka yake alikusudia kupata kitu. Atoe kwa imani atapokea
mabadiliko maana sadaka yake ilipata kibali. Tatizo sio kutoa sadaka bali
kufuata utaratibu na imani. Tusitoe kwa sababu ya utaratibu wa ibada. Tunatoa
kwa sababu tumepata msukumo utokao ndani wa kutoa na si kwa sababu umeambiwa
utoe.
Sikiliza hata
madhabahu ya shetani inataka sadaka ili ipate kujibu ndio maana wengine hutoa
watoto, ndugu, wazazi na hata viungo vya binadamu. Shetani ameiga mfumo huu ili
apofushe watu waone ni sawa na Mungu lakini sio kweli. Zab 20 inatueleza kuwa
kuna uhusiano mkubwa kati ya sadaka na majibu ya moyo wako.
2Fal 4:8-17 Elisha
alikwenda Shunemu, mama mmoja tajiri alimshurutisha ale chakula kwake. Lakini
yule mama alimwona Elisha kuwa ni mtumishi wa Mungu hivyo aliazimia na
kumwambia mumewe wajenge chumba ili wapate kumwifadhi Elisha akipita katika mji
huo. Sadaka ya kwanza ya yule mama hakumgusa Mungu bali ilimpa upako au maono
ya sadaka ambayo hiyo ndio itakayoachilia majibu ya matatizo aliokuwa nayo. Na
hiyo ndio sadaka ya chumba cha kulala alichokiandaa.
Ebr 11:4 Biblia
inatuambia tofauti ya sadaka ya Habili na Kaini haikuwa kwa vitu bali Habili
alitoa kwa imani lakini Kaini hakutoa kwa imani. Macho ya habili yaliona
matokeo.Hatimaye sadaka yake ikapata kibali. Wako watu mazoea shida yuko tayari
kupambana na matatizo kuliko kumwachia Yesu apate kushughulika nayo. Hivyo
wanataka sana dini kuliko Yesu. Ndio maana hata Yesu aliuliwa kwa sababu ya
dini.
Unapotoa sadaka
shughulikia utu wako wa ndani maana utu wako wa nje ni mavumbi. Pesa hazitoki
usipotoa pesa maana zina masikio ya kusikia, macho ya kuona ijapokuwa hazina
uhai zinajua zielekee wapi. Hivyo pesa ni roho ziendee rohoni ili ziwe zako.
Toa pesa ili upate pesa.
Barikiwa kwa
kunisikiliza
Na Henry Nicholaus
TUSIPOKUBALI
KUACHA NCHI TULIOPO NA KWENDA ILE ALIOTUAGIZA MUNGU HATUTAFANIKIWA
Mw 12: 1-4 Kuna
mahali ambapo Mungu amekuandalia ndio hiyo nchi. Usipofika hiyo nchi huwezi
kuona baraka. Ibrahim hakuweza kubarikiwa mpaka alipoamua kuondoka katika nchi
Bwana aliowaonyesha.Kabla Mungu kumwambia Ibrahim aondoke katika nchi alioishi
ilikuwa ya baba zake. Baba yake alikuwa muuza vinyago, hata Ibrahim naye
alifanya biashara hiyo. Hivyo hiyo nchi ilikuwa imefungwa na miungu ya baba
zake pamoja na laana za mizimu na mambo ya kimila. Hivyo Mungu asingeweza
kulikalisha jina lake eneo kama hilo. Ndio sababu ya kumwambia Ibrahimu
aondoke.
Ukitazama utaelewa
wakati Ibrahim anaondoka alikuwa na umri wa miaka 75 lakini ilimchukua miaka 24
kupata mzaliwa wake wa kwanza wa halali tena wa haki yaani Isaka. Sababu hii
ilitokana nchi aliokuwepo awali Ibrahimu isingeweza kumlea vyema mzaliwa wa kwanza
Ibrahim. Mw 12:2 Mungu anamwambia Ibrahimu kuwa atamfanya kuwa taifa kubwa na
kumbariki. Natamani uchunguze wewe mwenyewe hivi Mungu alishindwa nini kumfanya
taifa kubwa akiwa kwenye nchi aliokuwepo. Utagundua miungu ilokuwa inamiliki
nchi ya baba yake ndio ilikuwa kikwazo.
Yamkini mpaka leo
upo kwenye nchi za baba zako usipotoka huko Mungu hana msaada wa kukupa. Nchi
yako yaweza kuwa desturi ya maisha, mazoea fulani au mapokeo ulioyapata toka
kwa mababa zako. Haya yote ni nchi hivyo ni lazima ubadilike ili Yesu
akumilikishe ufalme kisha aingilie kati mambo yako.Kwa mfano tabia za kufanya
arubaini, ulevi, matambiko ya kimila, desturi ya kuishi nk. Hizi ni lazima
uziache sikiliza Mungu ni mwenye wivu hawezi kushare ufalme miungu mingine.
Lk 5:2-7 Yesu
anamwendea Petro alisameme kwenye mashua yake awezekuhubiri Petro anakubali.
Ndipo baada ya kumaliza kazi hiyo Yesu anamwambia Petro shusha nyavu kilindini.
Ukumbuke ni asubuhi, na jana yake waliangaika usiku kucha wasipate samaki
lakini Yesu alipomwambia licha sio kawaida ya wavuvi kuvua asubuhi biblia
inasema nyavu zilianza kukatika.Ina maanisha nini Petro hapo awali alikuwa
anavua katika miungu ya baba yake kwa sababu babaye alikuwa mvuvi naye alirithi
taaluma hiyo. Hiyo miungu ina viwango vya kufanya kazi haiwezi kila kitu. Hivyo
Yesu alipokuja alipomwambia Petro shusha nyavu zako ali ni asubuhi naye
akakubali ilionyesha Petro alikubali kutoka katika nchi aliokuwepo na kwenda
katika nchi aliomwonyesha Yesu.
Ndio maana Lk 5:8
Petro anamwambia Yesu ondoka kwangu mimi ni mwenye dhambi.Petro aligundua nchi
aliokuwepo si nzuri lakini ile Yesu aliokuwa anampeleka ni nchi ya kweli. Ewe
mama, baba, dada,kaka na kijana mwenzangu unayesoma waraka huu ni wakati muafaka
ambao Mungu ametaka wewe uhame katika nchi ya mazoea. Efe 1:3 inatuambia
umebarikiwa kwa baraka za rohoni kama umepewa kila kitu mbona unaishi maisha ya
shida hii ni kwa sababu hujaweza kujua utaratibu wa kuwa na hizo baraka.
Namshukuru Mungu
maana sasa umeelewa kutoka katika nchi uliopo. Jaribu kubadili mfumo wa maisha
uliokuwa nao kama kutokana na Roho Mtakatifu alivyokufundisha siku hii ya leo.
Maana Mungu anataka kukubariki katika masomo, kazi upandishwe cheo maradufu, uajiri
usiajiriwe, umiliki viwanda, magari, na pesa nyingi.
Chukua hatua
Barikiwa
Na Henry Nicholaus
No comments:
Post a Comment